Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Psalms

896 mistari · 16 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Bahari zimeinua, Ee Bwana, bahari zimeinua sauti zake; bahari zimeinua sauti za mawimbi yake.

  2. Yeye ni mkuu kuliko ngurumo ya maji makuu, ni mkuu kuliko mawimbi ya bahari: Bwana aishiye juu sana ni mkuu.

  3. Ee Bwana, sheria zako ni imara; utakatifu umepamba nyumba yako pasipo mwisho.

  4. Njooni, tumwimbie Bwana kwa furaha; tumfanyie kelele za shangwe Mwamba wa wokovu wetu.

  5. Tuje mbele zake kwa shukrani, tumtukuze kwa vinanda na nyimbo.

  6. Kwa kuwa Bwana ni Mungu mkuu, mfalme mkuu juu ya miungu yote.

  7. Mkononi mwake mna vilindi vya dunia, na vilele vya milima ni mali yake.

  8. Bahari ni yake, kwani ndiye aliifanya, na mikono yake iliumba nchi kavu.

  9. Njooni, tusujudu, tumwabudu, tupige magoti mbele za Bwana Muumba wetu,

  10. kwa maana yeye ndiye Mungu wetu, na sisi ni watu wa malisho yake, kondoo chini ya utunzaji wake. Kama mkiisikia sauti yake leo,

  11. msiifanye mioyo yenu migumu kama mlivyofanya kule Meriba, kama mlivyofanya siku ile kule Masa jangwani,

  12. ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu.

  13. Kwa miaka arobaini nilikasirikia kizazi kile, nikasema, “Hawa ni taifa ambalo mioyo yao imepotoka, nao hawajazijua njia zangu.”

  14. Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, “Kamwe hawataingia rahani mwangu.”

  15. Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.

  16. Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

  17. Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.

  18. Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

  19. Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.

  20. Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

  21. Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.

  22. Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.

  23. Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.

  24. Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.

  25. Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;