- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
circa 1010–970 BC
The Reign of David
David unites the tribes, conquers Jerusalem, and establishes Israel's golden age—even through deep personal failure.
Mistari ya kipindi hiki
- 1 Nyakati 16:20takriban 1042 KK
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
- 1 Nyakati 16:21takriban 1042 KK
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
- 1 Nyakati 16:22takriban 1042 KK
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
- 1 Nyakati 16:23takriban 1042 KK
Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
- 1 Nyakati 16:24takriban 1042 KK
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
- 1 Nyakati 16:25takriban 1042 KK
Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
- 1 Nyakati 16:26takriban 1042 KK
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
- 1 Nyakati 16:27takriban 1042 KK
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
- 1 Nyakati 16:28takriban 1042 KK
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
- 1 Nyakati 16:29takriban 1042 KK
mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
- 1 Nyakati 16:30takriban 1042 KK
Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
- 1 Nyakati 16:31takriban 1042 KK
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
- 1 Nyakati 16:32takriban 1042 KK
Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
- 1 Nyakati 16:33takriban 1042 KK
Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
- 1 Nyakati 16:34takriban 1042 KK
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
- 1 Nyakati 16:35takriban 1042 KK
Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
- 1 Nyakati 16:36takriban 1042 KK
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
- 1 Nyakati 16:37takriban 1042 KK
Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
- 1 Nyakati 16:38takriban 1042 KK
Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
- 1 Nyakati 16:39takriban 1042 KK
Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
- 1 Nyakati 16:40takriban 1042 KK
ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
- 1 Nyakati 16:41takriban 1042 KK
Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
- 1 Nyakati 16:42takriban 1042 KK
Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
- 1 Nyakati 16:43takriban 1042 KK
Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.
- 1 Nyakati 17:1takriban 1042 KK
Baada ya Daudi kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, akamwambia nabii Nathani, “Hebu tazama, mimi ninakaa kwenye nyumba nzuri iliyojengwa kwa mierezi, wakati Sanduku la Agano la Bwana liko ndani ya hema.”