Rukia maudhui

circa 800–400 BC

The Hebrew Prophets

God speaks through Isaiah, Jeremiah, and the minor prophets—calling Israel to repentance and foretelling the coming Messiah.

3,706 mistari · 14 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Isaya 31:5takriban 713 KK

    Kama ndege warukao, Bwana Mwenye Nguvu Zote ataukinga Yerusalemu; ataukinga na kuuokoa, atapita juu yake na kuufanya salama.”

  2. Isaya 31:6takriban 713 KK

    Mrudieni yeye ambaye nyumba ya Israeli imemwasi sana.

  3. Isaya 31:7takriban 713 KK

    Kwa kuwa katika siku ile kila mmoja wenu atazikataa sanamu za fedha na za dhahabu zilizotengenezwa kwa mikono yenu yenye dhambi.

  4. Isaya 31:8takriban 713 KK

    “Ashuru itaanguka kwa upanga ambao si wa mwanadamu; upanga usio wa kibinadamu utawaangamiza. Watakimbia mbele ya upanga na vijana wao wa kiume watafanyizwa kazi kwa lazima.

  5. Isaya 31:9takriban 713 KK

    Ngome zao zitaanguka kwa sababu ya hofu; kwa kuona bendera ya vita, majemadari wao watashikwa na hofu ya ghafula,” asema Bwana, ambaye moto wake uko Sayuni, nayo tanuru yake iko Yerusalemu.

  6. Isaya 32:1takriban 713 KK

    Tazama, mfalme atatawala kwa uadilifu na watawala watatawala kwa haki.

  7. Isaya 32:2takriban 713 KK

    Kila mtu atakuwa kama kivuli cha kujificha kutokana na upepo na kimbilio kutokana na dhoruba, kama vijito vya maji jangwani na kivuli cha mwamba mkubwa katika ardhi yenye kiu.

  8. Isaya 32:3takriban 713 KK

    Ndipo macho ya wale wanaoona hayatafumbwa tena, nayo masikio ya wale wanaosikia yatasikiliza.

  9. Isaya 32:4takriban 713 KK

    Moyo wa mtu mwenye hamaki utafahamu na kuelewa, nao ulimi wenye kigugumizi utanena kwa ufasaha.

  10. Isaya 32:5takriban 713 KK

    Mpumbavu hataitwa tena muungwana, wala mtu mbaya kabisa kupewa heshima ya juu.

  11. Isaya 32:6takriban 713 KK

    Kwa kuwa mpumbavu hunena upumbavu, moyo wake hushughulika na uovu: Hutenda mambo yasiyo ya kumcha Mungu, na hueneza habari za makosa kuhusu Bwana; yeye huwaacha wenye njaa bila kitu, na wenye kiu huwanyima maji.

  12. Isaya 32:7takriban 713 KK

    Taratibu za mtu mbaya kabisa ni ovu, hufanya mipango miovu ili kumwangamiza maskini kwa uongo, hata wakati ambapo hoja za mhitaji ni za haki.

  13. Isaya 32:8takriban 713 KK

    Lakini mtu muungwana hufanya mipango ya kiungwana, na kwa matendo ya kiungwana yeye hufanikiwa.

  14. Isaya 32:9takriban 713 KK

    Enyi wanawake wenye kuridhika sana, amkeni na mnisikilize. Enyi binti mnaojisikia kuwa salama, sikieni lile ninalotaka kuwaambia!

  15. Isaya 32:10takriban 713 KK

    Muda zaidi kidogo ya mwaka mmoja, ninyi mnaojisikia salama mtatetemeka, mavuno ya zabibu yatakoma na mavuno ya matunda hayatakuwepo.

  16. Isaya 32:11takriban 713 KK

    Tetemekeni, enyi wanawake wenye kuridhika, tetemekeni kwa hofu, enyi binti mnaojisikia salama! Vueni nguo zenu, vaeni nguo ya gunia viunoni mwenu.

  17. Isaya 32:12takriban 713 KK

    Pigeni matiti yenu kwa ajili ya mashamba mazuri, kwa ajili ya mizabibu iliyozaa vizuri

  18. Isaya 32:13takriban 713 KK

    na kwa ajili ya nchi ya watu wangu, nchi ambayo miiba na michongoma imemea: naam, ombolezeni kwa ajili ya nyumba zote za furaha na kwa ajili ya mji huu wenye kufanya sherehe.

  19. Isaya 32:14takriban 713 KK

    Ngome itaachwa, mji wenye kelele nyingi utahamwa, ngome ndani ya mji na mnara wa ulinzi vitakuwa ukiwa milele, mahali pazuri pa punda na malisho ya makundi ya kondoo,

  20. Isaya 32:15takriban 713 KK

    mpaka Roho amwagwe juu yetu kutoka juu, nalo jangwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba kuwa kama msitu.

  21. Isaya 32:16takriban 713 KK

    Haki itakaa katika jangwa, na uadilifu utakaa katika shamba lenye rutuba.

  22. Isaya 32:17takriban 713 KK

    Matunda ya haki yatakuwa amani, matokeo ya haki yatakuwa utulivu na matumaini milele.

  23. Isaya 32:18takriban 713 KK

    Watu wangu wataishi katika makao ya mahali pa amani, katika nyumba zilizo salama, katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.

  24. Isaya 32:19takriban 713 KK

    Hata kama mvua ya mawe iangushe msitu na mji ubomolewe kabisa,

  25. Isaya 32:20takriban 713 KK

    tazama jinsi utakavyobarikiwa, ukipanda mbegu yako katika kila kijito, na kuwaacha ngʼombe wako na punda wajilishe kwa uhuru.