Rukia maudhui

Creation Era

Creation & The Fall

God creates the heavens and earth, forming humanity in his image before sin enters the world.

138 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Mwanzo 4:21takriban 4003 KK

    Kaka yake aliitwa Yubali, aliyekuwa baba wa wote wapigao zeze na filimbi.

  2. Mwanzo 4:22takriban 4003 KK

    Pia Sila alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Tubali-Kaini ambaye alifua vifaa vya aina mbalimbali vya shaba na chuma. Naama alikuwa dada wa Tubali-Kaini.

  3. Mwanzo 4:23takriban 4003 KK

    Lameki akawaambia wake zake, “Ada na Sila nisikilizeni mimi; wake wa Lameki sikieni maneno yangu. Nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana mdogo kwa kuniumiza.

  4. Mwanzo 4:24takriban 4003 KK

    Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba, basi Lameki itakuwa mara sabini na saba.”

  5. Mwanzo 4:25takriban 4003 KK

    Adamu akakutana kimwili na mke wake tena, akamzaa mwana, akamwita Sethi, akisema, “Mungu amenijalia mwana mwingine badala ya Abeli, kwa kuwa Kaini alimuua.”

  6. Mwanzo 4:26takriban 3769 KK

    Naye Sethi akamzaa mwana, akamwita Enoshi. Wakati huo watu wakaanza kuliitia jina la Bwana.

  7. Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.

  8. Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”

  9. Mwanzo 5:3takriban 3874 KK

    Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.

  10. Mwanzo 5:4takriban 3874 KK

    Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.

  11. Mwanzo 5:5takriban 3074 KK

    Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.

  12. Mwanzo 5:6takriban 3769 KK

    Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.

  13. Mwanzo 5:7takriban 3769 KK

    Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.

  14. Mwanzo 5:8takriban 2962 KK

    Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.

  15. Mwanzo 5:9takriban 3679 KK

    Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.

  16. Mwanzo 5:10takriban 3679 KK

    Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.

  17. Mwanzo 5:11takriban 2864 KK

    Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.

  18. Mwanzo 5:12takriban 3609 KK

    Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.

  19. Mwanzo 5:13takriban 3609 KK

    Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.

  20. Mwanzo 5:14takriban 2769 KK

    Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.

  21. Mwanzo 5:15takriban 3544 KK

    Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.

  22. Mwanzo 5:16takriban 3544 KK

    Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.

  23. Mwanzo 5:17takriban 2714 KK

    Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.

  24. Mwanzo 5:18takriban 3382 KK

    Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.

  25. Mwanzo 5:19takriban 3382 KK

    Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.