Rukia maudhui

Creation Era

Creation & The Fall

God creates the heavens and earth, forming humanity in his image before sin enters the world.

138 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Mwanzo 5:20takriban 3382 KK

    Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.

  2. Mwanzo 5:21takriban 3317 KK

    Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.

  3. Mwanzo 5:22takriban 3317 KK

    Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.

  4. Mwanzo 5:23takriban 3017 KK

    Enoki aliishi jumla ya miaka 365.

  5. Mwanzo 5:24takriban 3017 KK

    Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.

  6. Mwanzo 5:25takriban 3130 KK

    Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.

  7. Mwanzo 5:26takriban 3130 KK

    Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.

  8. Mwanzo 5:27takriban 2348 KK

    Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.

  9. Mwanzo 5:28takriban 2948 KK

    Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.

  10. Mwanzo 5:29takriban 2948 KK

    Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”

  11. Mwanzo 5:30takriban 2948 KK

    Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.

  12. Mwanzo 5:31takriban 2353 KK

    Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.

  13. Mwanzo 5:32takriban 2448 KK

    Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.