Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Wicked

724 mistari · 18 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.

  2. Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.

  3. Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.

  4. Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.

  5. Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.

  6. Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.

  7. Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.

  8. Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.

  9. Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.

  10. Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.

  11. Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.

  12. Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.

  13. Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.

  14. Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”

  15. macheko ya mtu mwovu ni ya muda mfupi, nayo furaha ya wasiomcha Mungu hudumu kwa kitambo tu.

  16. Ingawa kujikweza kwake hufikia mbinguni na kichwa chake hugusa mawingu,

  17. ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe. Wale waliomwona watauliza, ‘Yuko wapi?’

  18. Kama ndoto hutoweka, wala hapatikani tena, amefukuziwa mbali kama maono ya usiku.

  19. Jicho lililomwona halitamwona tena; mahali pake hapatamwona tena.

  20. Watoto wake watalipa yote baba yao aliyowadhulumu maskini, nayo mikono yake itarudisha mali yote aliyonyangʼanya watu.

  21. Nguvu za ujana zilizoijaza mifupa yake, zitalala naye mavumbini.

  22. “Ingawa uovu ni mtamu kinywani mwake naye huuficha chini ya ulimi wake,

  23. ingawa hawezi kukubali kuuachia uende, lakini huuweka kinywani mwake.

  24. Hata hivyo chakula chake kitakuwa kichungu tumboni mwake, nacho kitakuwa sumu kali ya nyoka ndani yake.

  25. Atatema mali alizozimeza; Mungu atalifanya tumbo lake kuzitapika.