Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Wicked: Prosperity of

60 mistari · 18 vipengele

Mistari kuhusu Prosperity of

Chuja kwa kitabu
  1. Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.

  2. Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.

  3. Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.

  4. Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.

  5. Sauti za kutisha hujaa masikioni mwake; katika kufanikiwa kwake, wanyangʼanyi humshambulia.

  6. Hutangatanga, akitafuta chakula; anajua kwamba siku ya giza iko karibu.

  7. “Ingawa uso wake umefunikwa na mafuta kwa unene na kiuno chake kimevimba kwa kunenepa,

  8. Hatatajirika tena, nao utajiri wake hautadumu, wala mali zake hazitakuwa nyingi juu ya nchi.

  9. macheko ya mtu mwovu ni ya muda mfupi, nayo furaha ya wasiomcha Mungu hudumu kwa kitambo tu.

  10. Katikati ya wingi wa ustawi wake, dhiki itampata; taabu itamjia kwa nguvu zote.

  11. Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wakifikia umri wa uzee na kuendelea kuwa na nguvu?

  12. Huwaona watoto wao wakithibitika wakiwa wamewazunguka, wazao wao mbele za macho yao.

  13. Nyumba zao zi salama wala hakuna hofu; fimbo ya Mungu haiko juu yao.

  14. Madume yao ya ngʼombe huvyaza bila kushindwa kamwe; ngʼombe wao huzaa wala hawaharibu mimba.

  15. Huwatoa watoto wao nje kama kundi; wadogo wao huchezacheza.

  16. Huimba nyimbo kwa matari na kwa kinubi, nao huifurahia sauti ya filimbi.

  17. Huitumia miaka yao katika mafanikio nao hushuka kaburini kwa amani.

  18. Zaburi ya Daudi. Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu, wala usiwaonee wivu watendao mabaya,

  19. Nimemwona mtu mwovu na mkatili akistawi kama mwerezi wa Lebanoni,

  20. lakini alitoweka mara na hakuonekana, ingawa nilimtafuta, hakupatikana.

  21. Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa; wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia na kuwaachia wengine mali zao.

  22. Makaburi yao yatabaki kuwa nyumba zao za milele, makao yao vizazi vyote; ingawa walikuwa na mashamba na kuyaita kwa majina yao.

  23. Lakini mwanadamu, licha ya utajiri wake, hadumu; anafanana na mnyama aangamiaye.

  24. Hii ndiyo hatima ya wale wanaojitumainia wenyewe, pia ya wafuasi wao, waliothibitisha misemo yao.

  25. Kama kondoo, wamewekewa kwenda kaburini, nacho kifo kitawala. Wanyofu watawatawala asubuhi, maumbile yao yataozea kaburini, mbali na majumba yao makubwa ya fahari.