- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu God
Mistari muhimu ya Biblia
Ambaye aliumba mianga mikubwa, Fadhili zake zadumu milele.
Jua litawale mchana, Fadhili zake zadumu milele.
Mwezi na nyota vitawale usiku, Fadhili zake zadumu milele.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.
Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.
Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.
Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu, ni ya juu sana kwangu kuyafikia.
Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
Hutuma amri yake duniani, neno lake hukimbia kasi.
Anatandaza theluji kama sufu na kutawanya umande kama majivu.
Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe. Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?
Hutuma neno lake na kuviyeyusha, huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.
Msifuni yeye, enyi jua na mwezi, msifuni yeye, enyi nyota zote zingʼaazo.
Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu sana, na ninyi maji juu ya anga.
Vilisifu jina la Bwana kwa maana aliamuru navyo vikaumbwa.
Aliviweka mahali pake milele na milele, alitoa amri ambayo haibadiliki milele.
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:
wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.
kabla hajaumba dunia wala mashamba yake au vumbi lolote la dunia.
Nilikuwepo alipoziweka mbingu mahali pake, wakati alichora mstari wa upeo wa macho juu ya uso wa kilindi,