Rukia maudhui

circa 800–400 BC

The Hebrew Prophets

God speaks through Isaiah, Jeremiah, and the minor prophets—calling Israel to repentance and foretelling the coming Messiah.

3,706 mistari · 14 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Hosea 5:12takriban 780 KK

    Mimi ni kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa watu wa Yuda.

  2. Hosea 5:13takriban 780 KK

    “Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake, naye Yuda vidonda vyake, ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru, na kuomba msaada kwa mfalme mkuu. Lakini hawezi kukuponya, wala hawezi kukuponya vidonda vyako.

  3. Hosea 5:14takriban 780 KK

    Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu, kama simba mkubwa kwa Yuda. Nitawararua vipande vipande na kuondoka; nitawachukua mbali, na hakuna wa kuwaokoa.

  4. Hosea 5:15takriban 780 KK

    Kisha nitarudi mahali pangu mpaka watakapokubali kosa lao. Nao watautafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”

  5. Hosea 6:1takriban 780 KK

    “Njooni, tumrudie Bwana. Ameturarua vipande vipande lakini atatuponya; ametujeruhi lakini atatufunga majeraha yetu.

  6. Hosea 6:2takriban 780 KK

    Baada ya siku mbili atatufufua; katika siku ya tatu atatuinua, ili tuweze kuishi mbele zake.

  7. Hosea 6:3takriban 780 KK

    Tumkubali Bwana, tukaze kumkubali yeye. Kutokea kwake ni hakika kama vile kuchomoza kwa jua; atatujia kama mvua za masika, kama vile mvua za vuli ziinyweshavyo nchi.”

  8. Hosea 6:4takriban 780 KK

    “Nifanye nini nawe, Efraimu? Nifanye nini nawe, Yuda? Upendo wako ni kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao.

  9. Hosea 6:5takriban 780 KK

    Kwa hiyo ninawakata ninyi vipande vipande kwa kutumia manabii wangu; nimewaua ninyi kwa maneno ya kinywa changu, hukumu zangu zinawaka kama umeme juu yenu.

  10. Hosea 6:6takriban 780 KK

    Kwa maana nataka rehema, wala si dhabihu, kumkubali Mungu zaidi kuliko sadaka za kuteketezwa.

  11. Hosea 6:7takriban 780 KK

    Wamevunja Agano kama Adamu: huko hawakuwa waaminifu kwangu.

  12. Hosea 6:8takriban 780 KK

    Gileadi ni mji wenye watu waovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.

  13. Hosea 6:9takriban 780 KK

    Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.

  14. Hosea 6:10takriban 780 KK

    Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.

  15. Hosea 6:11takriban 780 KK

    “Pia kwa ajili yako, Yuda, mavuno yameamriwa. “Wakati wowote ningerejesha neema ya watu wangu,

  16. Hosea 7:1takriban 780 KK

    kila mara nilipotaka kumponya Israeli, dhambi za Efraimu zinafichuliwa na maovu ya Samaria yanafunuliwa. Wanafanya udanganyifu, wevi huvunja nyumba, maharamia hunyangʼanya barabarani,

  17. Hosea 7:2takriban 780 KK

    lakini hawafahamu kwamba ninakumbuka matendo yao yote mabaya. Dhambi zao zimewameza, ziko mbele zangu siku zote.

  18. Hosea 7:3takriban 780 KK

    “Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao, wakuu wao kwa uongo wao.

  19. Hosea 7:4takriban 780 KK

    Wote ni wazinzi, wanawaka kama tanuru ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea kuanzia kukanda unga hadi umekwisha kuumuka.

  20. Hosea 7:5takriban 780 KK

    Katika sikukuu ya mfalme wetu wakuu wanawaka kwa mvinyo, naye anawaunga mkono wenye mizaha.

  21. Hosea 7:6takriban 780 KK

    Mioyo yao ni kama tanuru, wanamwendea kwa hila. Hasira yao inafoka moshi usiku kucha, wakati wa asubuhi inalipuka kama miali ya moto.

  22. Hosea 7:7takriban 780 KK

    Wote ni moto kama tanuru; wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wake wote wanaanguka, wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.

  23. Hosea 7:8takriban 780 KK

    “Efraimu anajichanganya na mataifa; Efraimu ni mkate ambao haukuiva.

  24. Hosea 7:9takriban 780 KK

    Wageni wananyonya nguvu zake, lakini hafahamu hilo. Nywele zake zina mvi hapa na pale, lakini hana habari.

  25. Hosea 7:10takriban 780 KK

    Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake, lakini pamoja na haya yote harudi kwa Bwana Mungu wake wala kumtafuta.