- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
circa 1446 BC
Sinai & The Law
God meets Israel at Mount Sinai, reveals the Ten Commandments, and establishes the Tabernacle and the priestly covenant.
Mistari ya kipindi hiki
- Walawi 11:1takriban 1490 KK
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
- Walawi 11:2takriban 1490 KK
“Waambieni Waisraeli: ‘Kati ya wanyama wote waishio juu ya nchi, hawa ndio mtakaowala:
- Walawi 11:3takriban 1490 KK
Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.
- Walawi 11:4takriban 1490 KK
“ ‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.
- Walawi 11:5takriban 1490 KK
Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
- Walawi 11:6takriban 1490 KK
Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
- Walawi 11:7takriban 1490 KK
Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.
- Walawi 11:8takriban 1490 KK
Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.
- Walawi 11:9takriban 1490 KK
“ ‘Kuhusu viumbe wote wanaoishi ndani ya maji ya bahari na vijito, mtakula wale wote wenye mapezi na magamba.
- Walawi 11:10takriban 1490 KK
Lakini viumbe wote ndani ya bahari au vijito wasio na mapezi na magamba, wakiwa miongoni mwa makundi au viumbe wote ndani ya maji, hao ni machukizo kwenu.
- Walawi 11:11takriban 1490 KK
Nao watakuwa machukizo kwenu. Msile nyama yao, nayo mizoga yao itakuwa machukizo.
- Walawi 11:12takriban 1490 KK
Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba kitakuwa chukizo kwenu.
- Walawi 11:13takriban 1490 KK
“ ‘Wafuatao ndio ndege watakaokuwa machukizo kwenu, hivyo msiwale kwa sababu ni chukizo: tai, furukombe, kipungu,
- Walawi 11:14takriban 1490 KK
mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,
- Walawi 11:15takriban 1490 KK
aina zote za kunguru,
- Walawi 11:16takriban 1490 KK
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,
- Walawi 11:17takriban 1490 KK
bundi, mnandi, bundi mkubwa,
- Walawi 11:18takriban 1490 KK
mumbi, mwari, nderi,
- Walawi 11:19takriban 1490 KK
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
- Walawi 11:20takriban 1490 KK
“ ‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.
- Walawi 11:21takriban 1490 KK
Lakini wako viumbe wenye mabawa ambao hutembea kwa miguu minne mtakaowala: wale wenye vifundo katika miguu yao ya kurukaruka juu ya ardhi.
- Walawi 11:22takriban 1490 KK
Miongoni mwa hawa, mtakula nzige wa aina zote, senene, parare au panzi.
- Walawi 11:23takriban 1490 KK
Lakini viumbe wengine wote wenye mabawa na wenye miguu minne ni machukizo kwenu.
- Walawi 11:24takriban 1490 KK
“ ‘Mtajinajisi kwa wanyama hawa. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
- Walawi 11:25takriban 1490 KK
Yeyote atakayebeba mizoga ya viumbe hawa ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.