Rukia maudhui

circa 1446 BC

Sinai & The Law

God meets Israel at Mount Sinai, reveals the Ten Commandments, and establishes the Tabernacle and the priestly covenant.

1,657 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Walawi 11:1takriban 1490 KK

    Bwana akawaambia Mose na Aroni,

  2. Walawi 11:2takriban 1490 KK

    “Waambieni Waisraeli: ‘Kati ya wanyama wote waishio juu ya nchi, hawa ndio mtakaowala:

  3. Walawi 11:3takriban 1490 KK

    Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.

  4. Walawi 11:4takriban 1490 KK

    “ ‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.

  5. Walawi 11:5takriban 1490 KK

    Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.

  6. Walawi 11:6takriban 1490 KK

    Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.

  7. Walawi 11:7takriban 1490 KK

    Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.

  8. Walawi 11:8takriban 1490 KK

    Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.

  9. Walawi 11:9takriban 1490 KK

    “ ‘Kuhusu viumbe wote wanaoishi ndani ya maji ya bahari na vijito, mtakula wale wote wenye mapezi na magamba.

  10. Walawi 11:10takriban 1490 KK

    Lakini viumbe wote ndani ya bahari au vijito wasio na mapezi na magamba, wakiwa miongoni mwa makundi au viumbe wote ndani ya maji, hao ni machukizo kwenu.

  11. Walawi 11:11takriban 1490 KK

    Nao watakuwa machukizo kwenu. Msile nyama yao, nayo mizoga yao itakuwa machukizo.

  12. Walawi 11:12takriban 1490 KK

    Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba kitakuwa chukizo kwenu.

  13. Walawi 11:13takriban 1490 KK

    “ ‘Wafuatao ndio ndege watakaokuwa machukizo kwenu, hivyo msiwale kwa sababu ni chukizo: tai, furukombe, kipungu,

  14. Walawi 11:14takriban 1490 KK

    mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,

  15. Walawi 11:15takriban 1490 KK

    aina zote za kunguru,

  16. Walawi 11:16takriban 1490 KK

    mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,

  17. Walawi 11:17takriban 1490 KK

    bundi, mnandi, bundi mkubwa,

  18. Walawi 11:18takriban 1490 KK

    mumbi, mwari, nderi,

  19. Walawi 11:19takriban 1490 KK

    korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.

  20. Walawi 11:20takriban 1490 KK

    “ ‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.

  21. Walawi 11:21takriban 1490 KK

    Lakini wako viumbe wenye mabawa ambao hutembea kwa miguu minne mtakaowala: wale wenye vifundo katika miguu yao ya kurukaruka juu ya ardhi.

  22. Walawi 11:22takriban 1490 KK

    Miongoni mwa hawa, mtakula nzige wa aina zote, senene, parare au panzi.

  23. Walawi 11:23takriban 1490 KK

    Lakini viumbe wengine wote wenye mabawa na wenye miguu minne ni machukizo kwenu.

  24. Walawi 11:24takriban 1490 KK

    “ ‘Mtajinajisi kwa wanyama hawa. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.

  25. Walawi 11:25takriban 1490 KK

    Yeyote atakayebeba mizoga ya viumbe hawa ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.