Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 1 Timotheo 2:15takriban 65 BK

    Lakini mwanamke ataokolewa kwa kuzaa kwake, kama wakiendelea kudumu katika imani, upendo na utakatifu, pamoja na kuwa na kiasi.

  2. 1 Timotheo 3:1takriban 65 BK

    Hili ni neno la kuaminiwa, kwamba mtu akitamani kazi ya uangalizi, atamani kazi nzuri.

  3. 1 Timotheo 3:2takriban 65 BK

    Basi, imempasa mwangalizi awe mtu asiye na lawama, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi, anayejitawala, anayeheshimika, mkarimu, ajuaye kufundisha,

  4. 1 Timotheo 3:3takriban 65 BK

    asiwe mlevi, wala mkali bali awe mpole, asiwe mgomvi wala mpenda fedha.

  5. 1 Timotheo 3:4takriban 65 BK

    Lazima aweze kuisimamia nyumba yake mwenyewe vizuri na kuhakikisha kwamba watoto wake wanamtii na kuwa na heshima kwa kila njia.

  6. 1 Timotheo 3:5takriban 65 BK

    (Kwa maana kama mtu hajui jinsi ya kusimamia nyumba yake mwenyewe, atawezaje kuliangalia kanisa la Mungu?)

  7. 1 Timotheo 3:6takriban 65 BK

    Asiwe mtu aliyeokoka karibuni asije akajivuna na kuangukia kwenye hukumu ile ile ya ibilisi.

  8. 1 Timotheo 3:7takriban 65 BK

    Inampasa pia awe na sifa njema kwa watu walio nje, ili asije akalaumiwa na kuanguka kwenye mtego wa ibilisi.

  9. 1 Timotheo 3:8takriban 65 BK

    Vivyo hivyo, mashemasi nao wawe watu wanaostahili heshima, wasiwe wenye kauli mbili au wenye kujifurahisha kwa mvinyo, wala wanaotamani faida isiyo halali.

  10. 1 Timotheo 3:9takriban 65 BK

    Inawapasa kushikamana sana na ile siri ya imani kwa dhamiri safi.

  11. 1 Timotheo 3:10takriban 65 BK

    Ni lazima wapimwe kwanza; kisha kama hakuna neno dhidi yao, basi na waruhusiwe kuhudumu kama mashemasi.

  12. 1 Timotheo 3:11takriban 65 BK

    Vivyo hivyo, wake zao wawe wanawake wanaostahili heshima, wasio wasingiziaji, bali wawe na kiasi na waaminifu katika kila jambo.

  13. 1 Timotheo 3:12takriban 65 BK

    Shemasi awe mume wa mke mmoja na inampasa aweze kusimamia watoto wake na watu wa nyumbani mwake vyema.

  14. 1 Timotheo 3:13takriban 65 BK

    Wale ambao wamehudumu vyema katika huduma ya ushemasi hujipatia msimamo bora na ujasiri mkubwa katika imani yao ndani ya Kristo Yesu.

  15. 1 Timotheo 3:14takriban 65 BK

    Ingawa ninatarajia kuja kwako hivi karibuni, ninakuandikia maagizo haya sasa ili kwamba,

  16. 1 Timotheo 3:15takriban 65 BK

    kama nikikawia, utajua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, ambayo ndiyo kanisa la Mungu aliye hai, lililo nguzo na msingi wa kweli.

  17. 1 Timotheo 3:16takriban 65 BK

    Bila shaka yoyote, siri ya utauwa ni kubwa: Alidhihirishwa katika mwili wa kibinadamu, akathibitishwa kuwa na haki katika Roho, akaonekana na malaika, akahubiriwa miongoni mwa mataifa, akaaminiwa ulimwenguni, akachukuliwa juu katika utukufu.

  18. 1 Timotheo 4:1takriban 65 BK

    Roho asema waziwazi kwamba katika siku za mwisho baadhi ya watu wataiacha imani na kufuata roho zidanganyazo na mafundisho ya mashetani.

  19. 1 Timotheo 4:2takriban 65 BK

    Mafundisho kama hayo huja kupitia kwa waongo ambao ni wanafiki, hali dhamiri zao zikiungua kwa kuchomwa moto.

  20. 1 Timotheo 4:3takriban 65 BK

    Wao huwakataza watu wasioe na kuwaagiza wajiepushe na vyakula fulani, ambavyo Mungu aliviumba ili vipokewe kwa shukrani na wale wanaoamini na kuijua kweli.

  21. 1 Timotheo 4:4takriban 65 BK

    Kwa maana kila kitu alichokiumba Mungu ni chema, wala hakuna kitu chochote cha kukataliwa kama kikipokewa kwa shukrani,

  22. 1 Timotheo 4:5takriban 65 BK

    kwa sababu kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.

  23. 1 Timotheo 4:6takriban 65 BK

    Kama ukiwakumbusha ndugu mambo haya, utakuwa mtumishi mwema wa Kristo Yesu, uliyelelewa katika kweli ya imani na yale mafundisho mazuri uliyoyafuata.

  24. 1 Timotheo 4:7takriban 65 BK

    Usijishughulishe kamwe na hadithi za kipagani na masimulizi ya uongo ya wanawake wazee; badala yake, jizoeze kuwa mtauwa.

  25. 1 Timotheo 4:8takriban 65 BK

    Kwa maana mazoezi ya mwili yana faida kwa sehemu, lakini utauwa una faida katika mambo yote, yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa na ya ule ujao.