Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 2 Wathesalonike 3:3takriban 54 BK

    Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.

  2. 2 Wathesalonike 3:4takriban 54 BK

    Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.

  3. 2 Wathesalonike 3:5takriban 54 BK

    Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.

  4. 2 Wathesalonike 3:6takriban 54 BK

    Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.

  5. 2 Wathesalonike 3:7takriban 54 BK

    Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,

  6. 2 Wathesalonike 3:8takriban 54 BK

    wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.

  7. 2 Wathesalonike 3:9takriban 54 BK

    Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.

  8. 2 Wathesalonike 3:10takriban 54 BK

    Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”

  9. 2 Wathesalonike 3:11takriban 54 BK

    Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.

  10. 2 Wathesalonike 3:12takriban 54 BK

    Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.

  11. 2 Wathesalonike 3:13takriban 54 BK

    Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.

  12. 2 Wathesalonike 3:14takriban 54 BK

    Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.

  13. 2 Wathesalonike 3:15takriban 54 BK

    Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.

  14. 2 Wathesalonike 3:16takriban 54 BK

    Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.

  15. 2 Wathesalonike 3:17takriban 54 BK

    Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.

  16. 2 Wathesalonike 3:18takriban 54 BK

    Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.

  17. 1 Timotheo 1:1takriban 65 BK

    Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tumaini letu.

  18. 1 Timotheo 1:2takriban 65 BK

    Kwa Timotheo, mwanangu halisi katika imani: Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.

  19. 1 Timotheo 1:3takriban 65 BK

    Kama nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia, endelea kubaki Efeso, ili kwamba upate kuwaagiza watu wasiendelee kufundisha mafundisho ya uongo

  20. 1 Timotheo 1:4takriban 65 BK

    wala wasitoe muda wao kwa hadithi za kubuniwa na orodha za majina ya vizazi visivyo na mwisho, ambazo huchochea mabishano badala ya mpango wa Mungu utokanao na imani.

  21. 1 Timotheo 1:5takriban 65 BK

    Kusudi la maagizo haya ni upendo utokao katika moyo safi, dhamiri njema na imani ya kweli.

  22. 1 Timotheo 1:6takriban 65 BK

    Watu wengine wamepotoka kutoka haya na kugeukia majadiliano yasiyo na maana kwa kuwa,

  23. 1 Timotheo 1:7takriban 65 BK

    wanataka kuwa walimu wa sheria, lakini hawajui mambo yale wanayosema wala hayo wanayoyatumainia kwa uthabiti.

  24. 1 Timotheo 1:8takriban 65 BK

    Tunajua kwamba sheria ni njema ikiwa inatumika kwa halali kama ilivyokusudiwa.

  25. 1 Timotheo 1:9takriban 65 BK

    Lakini tunajua ya kuwa sheria si kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wavunja sheria na waasi, kwa ajili ya wasiomcha Mungu na wenye dhambi, wasio watakatifu na wanaokufuru; kwa wale wawauao baba zao au mama zao, kwa wauaji,