circa AD 48–96
Letters to the Churches
Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.
Mistari ya kipindi hiki
- 1 Timotheo 4:9takriban 65 BK
Hili ni neno la kuaminiwa tena lastahili kukubaliwa kabisa,
- 1 Timotheo 4:10takriban 65 BK
(nasi kwa ajili ya hili tunajitaabisha na kujitahidi), kwamba tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, hasa wale waaminio.
- 1 Timotheo 4:11takriban 65 BK
Mambo haya yaagize na kuyafundisha.
- 1 Timotheo 4:12takriban 65 BK
Mtu yeyote asikudharau kwa kuwa wewe ni kijana, bali uwe kielelezo kizuri kwa waumini katika usemi, mwenendo, upendo, imani na usafi.
- 1 Timotheo 4:13takriban 65 BK
Fanya bidii kusoma Maandiko hadharani, kuhubiri na kufundisha, mpaka nitakapokuja.
- 1 Timotheo 4:14takriban 65 BK
Usiache kutumia kipawa kilicho ndani yako, ambacho ulipewa kwa neno la unabii wakati wazee walikuwekea mikono.
- 1 Timotheo 4:15takriban 65 BK
Uwe na bidii katika mambo haya; ujitolee kwa ajili ya mambo haya kikamilifu, ili kila mtu aone kuendelea kwako.
- 1 Timotheo 4:16takriban 65 BK
Jilinde sana nafsi yako na mafundisho yako. Dumu katika hayo, kwa maana kwa kufanya hivyo, utajiokoa wewe mwenyewe pamoja na wale wanaokusikia.
- 1 Timotheo 5:1takriban 65 BK
Usimkemee mzee kwa ukali bali umshawishi kama vile angekuwa ni baba yako. Uwatendee vijana kama vile ndugu zako;
- 1 Timotheo 5:2takriban 65 BK
nao wanawake wazee uwatendee kama mama zako, na wanawake vijana kama dada zako, katika usafi wote.
- 1 Timotheo 5:3takriban 65 BK
Waheshimu wanawake wajane ambao ni wajane kweli kweli.
- 1 Timotheo 5:4takriban 65 BK
Kama mjane ana watoto ama wajukuu, hawa inawapasa awali ya yote wajifunze kutimiza wajibu wao wa kumcha Mungu katika matendo kwa kuwatunza wale wa jamaa zao wenyewe, na hivyo wawarudishie wema waliowatendea wazazi wao, kwa kuwa hivi ndivyo impendezavyo Mungu.
- 1 Timotheo 5:5takriban 65 BK
Mwanamke ambaye ni mjane kweli kweli, yaani, yeye aliyebaki peke yake huweka tumaini lake kwa Mungu naye hudumu katika maombi usiku na mchana akimwomba Mungu ili amsaidie.
- 1 Timotheo 5:6takriban 65 BK
Lakini mjane aishiye kwa anasa amekufa, ingawa anaishi.
- 1 Timotheo 5:7takriban 65 BK
Wape watu maagizo haya pia, ili asiwepo yeyote wa kulaumiwa.
- 1 Timotheo 5:8takriban 65 BK
Kama mtu hawatunzi wale wa jamaa yake, hasa wale wa nyumbani mwake mwenyewe, ameikana imani, tena ni mbaya kuliko yeye asiyeamini.
- 1 Timotheo 5:9takriban 65 BK
Mjane yeyote asiwekwe kwenye orodha ya wajane isipokuwa awe ametimiza umri wa miaka sitini, na ambaye alikuwa mke wa mume mmoja,
- 1 Timotheo 5:10takriban 65 BK
awe ameshuhudiwa kwa matendo yake mema, aliyewalea watoto wake vizuri, aliye mkarimu, aliyewanawisha watakatifu miguu, aliyewasaidia wenye shida na aliyejitolea kwa ajili ya matendo mema ya kila namna.
- 1 Timotheo 5:11takriban 65 BK
Lakini kwa habari za wajane vijana usiwaweke kwenye orodha hiyo, maana tamaa zao za kimaumbile zikizidi kule kujitoa kwao kwa Kristo, watataka kuolewa tena.
- 1 Timotheo 5:12takriban 65 BK
Nao kwa njia hiyo watajiletea hukumu kwa kukiuka ahadi yao ya kwanza.
- 1 Timotheo 5:13takriban 65 BK
Zaidi ya hayo, wajane kama hao huwa na tabia ya uvivu wakizurura nyumba kwa nyumba, wala hawawi wavivu tu, bali pia huwa wasengenyaji, wajiingizao katika mambo yasiyowahusu na kusema mambo yasiyowapasa kusema.
- 1 Timotheo 5:14takriban 65 BK
Hivyo nawashauri wajane vijana waolewe, wazae watoto na wasimamie nyumba zao, wasije wakampa adui nafasi ya kutushutumu.
- 1 Timotheo 5:15takriban 65 BK
Kwa maana kwa kweli wajane wengine wamepotoka ili kumfuata Shetani.
- 1 Timotheo 5:16takriban 65 BK
Lakini kama mwanamke yeyote aaminiye ana wajane katika jamaa yake, inampasa awasaidie wala si kuwaacha wakililemea kanisa, ili kanisa liweze kuwasaidia wale ambao ni wajane kweli kweli.
- 1 Timotheo 5:17takriban 65 BK
Wazee wa kanisa wanaoongoza shughuli za kanisa vizuri wanastahili heshima mara mbili, hasa wale ambao kazi yao ni kuhubiri na kufundisha.