circa AD 48–96
Letters to the Churches
Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.
Mistari ya kipindi hiki
- Wagalatia 5:19takriban 58 BK
Basi matendo ya mwili ni dhahiri nayo ni haya: Uasherati, uchafu, ufisadi,
- Wagalatia 5:20takriban 58 BK
kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
- Wagalatia 5:21takriban 58 BK
husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine yanayofanana na hayo. Nawaonya, kama nilivyokwisha kuwaonya kabla, kwamba watu watendao mambo kama hayo, hawataurithi Ufalme wa Mungu.
- Wagalatia 5:22takriban 58 BK
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
- Wagalatia 5:23takriban 58 BK
upole na kiasi. Katika mambo kama haya hakuna sheria.
- Wagalatia 5:24takriban 58 BK
Wote walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili na shauku zake pamoja na tamaa zake.
- Wagalatia 5:25takriban 58 BK
Kwa kuwa tunaishi kwa Roho, basi, tuenende kwa Roho.
- Wagalatia 5:26takriban 58 BK
Tusijisifu bure, tukichokozana na kuoneana wivu.
- Wagalatia 6:1takriban 58 BK
Ndugu zangu, ikiwa mtu ameghafilika akatenda dhambi, basi ninyi mlio wa rohoni, mrejesheni upya mtu huyo kwa roho ya upole. Lakini jihadharini, ili ninyi wenyewe msije mkajaribiwa.
- Wagalatia 6:2takriban 58 BK
Chukulianeni mizigo ninyi kwa ninyi, nanyi kwa njia hii mtatimiza sheria ya Kristo.
- Wagalatia 6:3takriban 58 BK
Kama mtu yeyote akijiona kuwa yeye ni bora na kumbe sivyo, basi mtu huyo anajidanganya mwenyewe.
- Wagalatia 6:4takriban 58 BK
Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo aweze kujisifu, bila kujilinganisha na mtu mwingine.
- Wagalatia 6:5takriban 58 BK
Kwa maana, kila mtu atauchukua mzigo wake mwenyewe.
- Wagalatia 6:6takriban 58 BK
Basi, yeye afundishwaye katika neno na amshirikishe mwalimu wake mema yote.
- Wagalatia 6:7takriban 58 BK
Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi. Kwa kuwa kile apandacho mtu ndicho atakachovuna.
- Wagalatia 6:8takriban 58 BK
Apandaye kwa mwili, katika mwili wake atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye katika Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele.
- Wagalatia 6:9takriban 58 BK
Hivyo, tusichoke katika kutenda mema, kwa kuwa tutavuna kwa wakati wake tusipokata tamaa.
- Wagalatia 6:10takriban 58 BK
Kwa hiyo, kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema, hasa wale wa jamaa ya waaminio.
- Wagalatia 6:11takriban 58 BK
Angalieni herufi kubwa nitumiazo ninapowaandikia kwa mkono wangu mwenyewe!
- Wagalatia 6:12takriban 58 BK
Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili wanataka wawalazimishe kutahiriwa. Sababu pekee ya kufanya hivyo ni kuepuka kuteswa kwa ajili ya msalaba wa Kristo.
- Wagalatia 6:13takriban 58 BK
Hata wale waliotahiriwa wenyewe hawaitii sheria, lakini wanataka ninyi mtahiriwe ili wapate kujivuna kwa habari ya miili yenu.
- Wagalatia 6:14takriban 58 BK
Mungu apishie mbali nisije nikajivunia kitu chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa yeye ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu.
- Wagalatia 6:15takriban 58 BK
Kwa maana katika Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa si kitu, bali kule kuwa kiumbe kipya ni kila kitu!
- Wagalatia 6:16takriban 58 BK
Amani na rehema viwe na wote wanaofuata kanuni hii, na juu ya Israeli wa Mungu.
- Wagalatia 6:17takriban 58 BK
Hatimaye, tangu sasa mtu yeyote asinitaabishe, kwa maana nachukua katika mwili wangu chapa zake Yesu.