Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Wagalatia 3:29takriban 58 BK

    Nanyi mkiwa ni mali ya Kristo, basi ninyi ni wa uzao wa Abrahamu na warithi sawasawa na ile ahadi.

  2. Wagalatia 4:1takriban 58 BK

    Lile nisemalo ni kwamba wakati wote mrithi bado ni mtoto, hana tofauti na mtumwa, ingawa ndiye mmiliki wa mali yote.

  3. Wagalatia 4:2takriban 58 BK

    Yeye huwa yuko chini ya uangalizi wa walezi na wadhamini mpaka ufike wakati uliowekwa na baba yake.

  4. Wagalatia 4:3takriban 58 BK

    Vivyo hivyo na sisi, tulipokuwa bado watoto wadogo, tulikuwa utumwani chini ya taratibu za kawaida za ulimwengu.

  5. Wagalatia 4:4takriban 58 BK

    Lakini ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe, ambaye alizaliwa na mwanamke, akazaliwa chini ya sheria,

  6. Wagalatia 4:5takriban 58 BK

    kusudi awakomboe wale waliokuwa chini ya sheria, ili tupate kupokea zile haki kamili za kufanywa watoto wa Mungu.

  7. Wagalatia 4:6takriban 58 BK

    Kwa sababu ninyi ni watoto wa Mungu, Mungu amemtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, anayelia, “Abba, Baba.”

  8. Wagalatia 4:7takriban 58 BK

    Kwa hiyo, wewe si mtumwa tena, bali ni mtoto, kwa kuwa wewe ni mtoto, Mungu amekufanya wewe pia kuwa mrithi kwa kupitia Kristo.

  9. Wagalatia 4:8takriban 58 BK

    Zamani, mlipokuwa hammjui Mungu, mlikuwa watumwa wa viumbe ambavyo kwa asili si Mungu.

  10. Wagalatia 4:9takriban 58 BK

    Lakini sasa kwa kuwa mmemjua Mungu, au zaidi mmejulikana na Mungu, inakuwaje mnarejea tena katika zile kanuni za kwanza zenye udhaifu na upungufu? Mnataka ziwafanye tena watumwa?

  11. Wagalatia 4:10takriban 58 BK

    Mnaadhimisha siku maalum, miezi, nyakati na miaka!

  12. Wagalatia 4:11takriban 58 BK

    Nina hofu juu yenu, kwamba kazi niliyofanya kwa ajili yenu inaweza kuwa nimejitaabisha bure.

  13. Wagalatia 4:12takriban 58 BK

    Ndugu zangu, nawasihi mwe kama mimi, kwa sababu mimi nimekuwa kama ninyi. Hamkunitendea jambo lolote baya.

  14. Wagalatia 4:13takriban 58 BK

    Ninyi mwajua kwamba ni kwa ajili ya udhaifu wangu niliwahubiria Injili.

  15. Wagalatia 4:14takriban 58 BK

    Ingawa hali yangu iliwatia majaribuni, hamkunidharau wala kunidhihaki, bali mlinikaribisha kama malaika wa Mungu, kama vile Kristo Yesu.

  16. Wagalatia 4:15takriban 58 BK

    Ile hali ya furaha mliyokuwa nayo imekwenda wapi? Naweza kushuhudia kwamba, kama ingewezekana mngengʼoa macho yenu na kunipa mimi.

  17. Wagalatia 4:16takriban 58 BK

    Je, sasa nimekuwa adui yenu kwa kuwaambia kweli?

  18. Wagalatia 4:17takriban 58 BK

    Hao wana shauku ya kuwapata lakini si kwa kusudi zuri. Wanachotaka ni kuwatenga mbali nasi, ili ninyi mpate kuwaonea wao shauku.

  19. Wagalatia 4:18takriban 58 BK

    Ni vizuri wakati wote kuwa na shauku kwa ajili ya kusudi zuri, si wakati nikiwa pamoja nanyi tu.

  20. Wagalatia 4:19takriban 58 BK

    Watoto wangu wapendwa, ambao kwa mara nyingine ninawaonea utungu, ninatamani kwamba Kristo aumbike ndani yenu.

  21. Wagalatia 4:20takriban 58 BK

    Natamani kama ningekuwa pamoja nanyi sasa, pengine ningebadilisha sauti yangu. Kwa maana nina wasiwasi kwa ajili yenu.

  22. Wagalatia 4:21takriban 58 BK

    Niambieni, ninyi mnaotaka kuwa chini ya sheria, je, hamjui sheria inavyosema?

  23. Wagalatia 4:22takriban 58 BK

    Kwa maana imeandikwa kwamba Abrahamu alikuwa na wana wawili, mmoja wa mwanamke mtumwa na wa pili wa mwanamke huru.

  24. Wagalatia 4:23takriban 58 BK

    Lakini, mtoto wa mwanamke mtumwa alizaliwa kwa mapenzi ya mwili, na yule mwingine wa mwanamke huru alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu.

  25. Wagalatia 4:24takriban 58 BK

    Mambo haya yanaweza kuchukuliwa kama mfano. Kwa maana hao wanawake wawili ni mfano wa maagano mawili: Agano la kwanza, ni lile lililofanyika katika Mlima Sinai, lizaalo watoto wa utumwa. Hili ndilo huyo Hagari.