circa AD 48–96
Letters to the Churches
Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.
Mistari ya kipindi hiki
- Wagalatia 3:4takriban 58 BK
Je, mlipata mateso kiasi hicho bure? Ni kama kweli yalikuwa bure!
- Wagalatia 3:5takriban 58 BK
Je, Mungu huwapa Roho wake na kufanya miujiza katikati yenu kwa sababu mnatii sheria, au kwa sababu mnaamini kile mlichosikia?
- Wagalatia 3:6takriban 58 BK
Kama vile “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
- Wagalatia 3:7takriban 58 BK
Fahamuni basi kwamba wale walio na imani, hao ndio watoto wa Abrahamu.
- Wagalatia 3:8takriban 58 BK
Maandiko yakitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa Mataifa kwa imani, alitangulia kumtangazia Abrahamu Injili akisema kwamba, “Kwa kupitia kwako mataifa yote yatabarikiwa.”
- Wagalatia 3:9takriban 58 BK
Kwa sababu hii, wale wote wanaoamini wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mtu wa imani.
- Wagalatia 3:10takriban 58 BK
Kwa maana wote wanaotumainia matendo ya sheria wako chini ya laana, kwa kuwa imeandikwa, “Alaaniwe kila mtu asiyeshikilia kutii mambo yote yaliyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.”
- Wagalatia 3:11takriban 58 BK
Basi ni dhahiri kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa kushikilia sheria, kwa maana, “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
- Wagalatia 3:12takriban 58 BK
Lakini sheria haitegemei imani. Kinyume chake, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
- Wagalatia 3:13takriban 58 BK
Kristo alitukomboa kutoka laana ya sheria kwa kufanyika laana kwa ajili yetu, kwa maana imeandikwa, “Amelaaniwa yeye aangikwaye juu ya mti.”
- Wagalatia 3:14takriban 58 BK
Alitukomboa ili kwamba baraka aliyopewa Abrahamu ipate kuwafikia watu wa Mataifa kwa njia ya Kristo Yesu, ili kwa imani tupate kupokea ile ahadi ya Roho.
- Wagalatia 3:15takriban 58 BK
Ndugu zangu, nataka nitoe mfano kutoka maisha ya kila siku. Kama vile hakuna mtu awezaye kutangua au kuongeza kitu katika agano la mtu ambalo limekwisha kuthibitishwa, vivyo hivyo kwa hali kama hii.
- Wagalatia 3:16takriban 58 BK
Ahadi zilinenwa kwa Abrahamu na kwa mzao wake. Maandiko hayasemi “kwa wazao,” likimaanisha watu wengi, bali “kwa mzao wako,” yaani mtu mmoja, ndiye Kristo.
- Wagalatia 3:17takriban 58 BK
Ninachotaka kusema ni kwamba, sheria, ambayo ilitolewa miaka 430 baadaye, haitangui Agano lililothibitishwa na Mungu ili kuibatilisha ahadi ile.
- Wagalatia 3:18takriban 58 BK
Kwa maana kama urithi hupatikana kwa sheria, basi hautegemei tena ahadi, lakini Mungu kwa neema yake alimpa Abrahamu urithi kwa njia ya ahadi.
- Wagalatia 3:19takriban 58 BK
Kwa nini basi iwepo sheria? Sheria iliwekwa kwa sababu ya makosa mpaka atakapokuja yule Mzao wa Abrahamu, ambaye alitajwa katika ile ahadi. Sheria iliamriwa na malaika kwa mkono wa mpatanishi.
- Wagalatia 3:20takriban 58 BK
Basi mpatanishi huhusisha zaidi ya upande mmoja, lakini Mungu ni mmoja.
- Wagalatia 3:21takriban 58 BK
Je basi, sheria inapingana na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa maana kama sheria iliyotolewa ingeweza kuwapa watu uzima, basi haki ingepatikana kwa njia ya sheria.
- Wagalatia 3:22takriban 58 BK
Lakini Maandiko yamefanya vitu vyote vifungwe chini ya nguvu ya dhambi, ili yale yaliyoahidiwa kwa njia ya imani katika Yesu Kristo yapate kupewa wale wanaoamini.
- Wagalatia 3:23takriban 58 BK
Kabla imani hii haijaja tulikuwa tumewekwa chini ya sheria, tumefungwa mpaka ile imani ifunuliwe.
- Wagalatia 3:24takriban 58 BK
Hivyo, sheria ilikuwa kiongozi kutufikisha kwa Kristo, ili tupate kuhesabiwa haki kwa imani.
- Wagalatia 3:25takriban 58 BK
Lakini sasa kwa kuwa ile imani imekuja, hatusimamiwi tena na sheria.
- Wagalatia 3:26takriban 58 BK
Kwa maana ninyi nyote mmekuwa watoto wa Mungu katika Kristo Yesu kwa njia ya imani.
- Wagalatia 3:27takriban 58 BK
Kwa maana wote mliobatizwa ndani ya Kristo, mmemvaa Kristo.
- Wagalatia 3:28takriban 58 BK
Wala hakuna tena Myahudi au Myunani, mtumwa au mtu huru, mwanaume wala mwanamke, maana nyote mmekuwa wamoja ndani ya Kristo Yesu.