Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Death

177 mistari · 6 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Mwanadamu mwenye utajiri bila ufahamu ni kama wanyama waangamiao.

  2. Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.

  3. Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.

  4. Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.

  5. Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.

  6. Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!

  7. Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.

  8. nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.

  9. Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?

  10. Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?

  11. Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?

  12. Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.

  13. Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?

  14. kwa kuwa anajua tulivyoumbwa, anakumbuka kwamba sisi tu mavumbi.

  15. Kuhusu mwanadamu, siku zake ni kama majani, anachanua kama ua la shambani;

  16. upepo huvuma juu yake nalo hutoweka, mahali pake hapalikumbuki tena.

  17. Matendo mabaya ya mtu mwovu humnasa yeye mwenyewe; kamba za dhambi yake humkamata kwa nguvu.

  18. Atakufa kwa kukosa nidhamu, akipotoshwa kwa upumbavu wake mwenyewe.

  19. Mtu mwenye hekima ana macho katika kichwa chake, lakini mpumbavu anatembea gizani; lakini nikaja kuona kwamba wote wawili hatima yao inafanana.

  20. Kisha nikafikiri moyoni mwangu, “Hatima ya mpumbavu itanipata mimi pia. Nitafaidi nini basi kwa kuwa na hekima?” Nikasema moyoni mwangu, “Hili nalo ni ubatili.”

  21. Kwa maana kwa mtu mwenye hekima, kama ilivyo kwa mpumbavu, hatakumbukwa kwa muda mrefu, katika siku zijazo wote watasahaulika. Kama vile ilivyo kwa mpumbavu, mtu mwenye hekima pia lazima atakufa!

  22. Kwa hiyo nikachukia maisha, kwa sababu kazi inayofanyika chini ya jua ilikuwa masikitiko kwangu. Yote hayo ni ubatili, ni kukimbiza upepo.

  23. Nikachukia kila kitu nilichokuwa nimetaabikia chini ya jua, kwa sababu ni lazima nimwachie yule ajaye baada yangu.

  24. Hatima ya mwanadamu ni kama ile ya wanyama; wote wana mwisho unaofanana: Jinsi anavyokufa mnyama, ndivyo anavyokufa mwanadamu. Wote wana pumzi inayofanana; mwanadamu hana cha zaidi kuliko mnyama. Kila kitu ni ubatili.

  25. Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi.