Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Death

177 mistari · 6 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Ni mara ngapi huwa kama majani makavu mbele ya upepo, kama makapi yachukuliwayo na dhoruba?

  2. Mtu mmoja hufa akiwa na nguvu zake kamili, akiwa salama na mwenye raha kamili,

  3. mwili wake ukiwa umenawiri, nayo mifupa yake ikiwa imejaa mafuta ndani yake.

  4. Mtu mwingine hufa katika uchungu wa nafsi, akiwa hajafurahia kamwe jambo lolote zuri.

  5. Hao wote hulala mavumbini, nao mabuu huwafunika wote.

  6. Hupelekwa kaburini, nao ulinzi ukawekwa kwenye kaburi lake.

  7. Udongo ulio bondeni ni mtamu kwake; watu wote watamfuata, nao umati wa watu usiohesabika umemtangulia.

  8. Yeye hulala akiwa tajiri, lakini ndiyo mara ya mwisho; afunguapo macho yake, yote yametoweka.

  9. Vitisho humjia kama mafuriko; dhoruba humkumba ghafula usiku.

  10. Upepo mkali wa mashariki humchukua, naye hutoweka; humzoa kutoka mahali pake.

  11. Humvurumisha bila huruma, huku akikimbia kasi kukwepa nguvu zake.

  12. Upepo humpigia makofi kwa dharau, na kumfukuza atoke mahali pake.

  13. Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,

  14. wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.

  15. Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.

  16. Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?

  17. Zaburi ya Daudi. Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu, wala usiwaonee wivu watendao mabaya,

  18. kwa maana kama majani watanyauka mara, kama mimea ya kijani watakufa mara.

  19. Kwa maana waovu watakatiliwa mbali, bali wale wanaomtumaini Bwana watairithi nchi.

  20. Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana, ingawa utawatafuta, hawataonekana.

  21. Nimemwona mtu mwovu na mkatili akistawi kama mwerezi wa Lebanoni,

  22. lakini alitoweka mara na hakuonekana, ingawa nilimtafuta, hakupatikana.

  23. ili kwamba aishi milele na asione uharibifu.

  24. Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa; wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia na kuwaachia wengine mali zao.

  25. atajiunga na kizazi cha baba zake, ambao hawataona kamwe nuru ya uzima.