Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Filemoni 1:18takriban 64 BK

    Kama amekukosea lolote au kama unamdai chochote, nidai mimi.

  2. Filemoni 1:19takriban 64 BK

    Ni mimi Paulo, ninayeandika waraka huu kwa mkono wangu mwenyewe. Nitakulipa. Sitaji kwamba nakudai hata nafsi yako.

  3. Filemoni 1:20takriban 64 BK

    Ndugu yangu, natamani nipate faida kwako katika Bwana, uuburudishe moyo wangu katika Kristo.

  4. Filemoni 1:21takriban 64 BK

    Nikiwa na hakika ya utii wako, nakuandikia, nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya yale ninayokuomba.

  5. Filemoni 1:22takriban 64 BK

    Jambo moja zaidi: Niandalie chumba cha wageni, kwa kuwa nataraji kurudishwa kwenu kama jibu la maombi yenu.

  6. Filemoni 1:23takriban 64 BK

    Epafra, aliye mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu, anakusalimu.

  7. Filemoni 1:24takriban 64 BK

    Vivyo hivyo Marko, Aristarko, Dema na Luka, watendakazi wenzangu wanakusalimu.

  8. Filemoni 1:25takriban 64 BK

    Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.

  9. Waebrania 1:1takriban 64 BK

    Zamani Mungu alisema na baba zetu kwa njia ya manabii mara nyingi na kwa njia mbalimbali,

  10. Waebrania 1:2takriban 64 BK

    lakini katika siku hizi za mwisho anasema nasi kwa njia ya Mwanawe, ambaye amemweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia kwake aliuumba ulimwengu.

  11. Waebrania 1:3takriban 64 BK

    Mwana ni mngʼao wa utukufu wa Mungu na mfano halisi wa nafsi yake, akivihifadhi vitu vyote kwa neno lake lenye uweza. Akiisha kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Aliye Mkuu huko mbinguni.

  12. Waebrania 1:4takriban 64 BK

    Kwa hiyo alifanyika bora kuliko malaika, kama jina alilorithi lilivyo bora kuliko lao.

  13. Waebrania 1:5takriban 64 BK

    Kwa maana ni malaika yupi ambaye wakati wowote Mungu alipata kumwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa?” Au tena, “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu?”

  14. Waebrania 1:6takriban 64 BK

    Tena, Mungu amletapo mzaliwa wake wa kwanza ulimwenguni, anasema, “Malaika wote wa Mungu na wamsujudu.”

  15. Waebrania 1:7takriban 64 BK

    Anenapo kuhusu malaika asema, “Huwafanya malaika wake kuwa pepo, watumishi wake kuwa miali ya moto.”

  16. Waebrania 1:8takriban 64 BK

    Lakini kwa habari za Mwana asema, “Kiti chako cha enzi, Ee Mungu, kitadumu milele na milele, nayo haki itakuwa fimbo ya utawala ya ufalme wako.

  17. Waebrania 1:9takriban 64 BK

    Umependa haki na kuchukia uovu; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekuweka juu ya wenzako kwa kukupaka mafuta ya furaha.”

  18. Waebrania 1:10takriban 64 BK

    Pia asema, “Hapo mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.

  19. Waebrania 1:11takriban 64 BK

    Hizo zitatoweka, lakini wewe utadumu; zote zitachakaa kama vazi.

  20. Waebrania 1:12takriban 64 BK

    Utazikungʼutakungʼuta kama joho, nazo zitachakaa kama vazi. Lakini wewe hubadiliki, nayo miaka yako haikomi kamwe.”

  21. Waebrania 1:13takriban 64 BK

    Je, ni kwa malaika yupi ambaye Mungu amepata kumwambia wakati wowote, “Keti mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako”?

  22. Waebrania 1:14takriban 64 BK

    Je, malaika wote si roho watumikao, waliotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu?

  23. Waebrania 2:1takriban 64 BK

    Kwa hiyo, imetupasa kuwa waangalifu sana kuhusu kile tulichosikia, ili tusije tukakiacha.

  24. Waebrania 2:2takriban 64 BK

    Kwa kuwa kama ujumbe ulionenwa na malaika ulikuwa imara, na kila uasi na kutokutii kulipata adhabu ya haki,

  25. Waebrania 2:3takriban 64 BK

    je, sisi tutapaje kupona kama tusipojali wokovu mkuu namna hii? Wokovu huu, ambao mwanzo ulitangazwa na Bwana, ulithibitishwa kwetu na wale waliomsikia.