Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Temptation

346 mistari · 52 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine na miaka yako kwa aliye mkatili,

  2. wageni wasije wakasherehekea utajiri wako na jitihada yako ikatajirisha nyumba ya mwanaume mwingine.

  3. Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu, wakati nyama na mwili wako vimechakaa.

  4. Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu! Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!

  5. Sikuwatii walimu wangu wala kuwasikiliza wakufunzi wangu.

  6. Nimefika ukingoni mwa maangamizi kabisa katikati ya kusanyiko lote.”

  7. Kunywa maji kutoka kwenye kisima chako mwenyewe, maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe.

  8. Je, chemchemi zako zifurike katika barabara za mji na vijito vyako vya maji viwanjani?

  9. Na viwe vyako mwenyewe, kamwe visishirikishwe wageni.

  10. Chemchemi yako na ibarikiwe na umfurahie mke wa ujana wako.

  11. Kulungu jike apendaye, kulungu mzuri: matiti yake na yakutosheleze siku zote, nawe utekwe daima na upendo wake.

  12. Kwa nini mwanangu, utekwe na mwanamke kahaba? Kwa nini ukumbatie kifua cha mke wa mwanaume mwingine?

  13. Kwa maana njia za mtu ni wazi kabisa mbele za Bwana, naye huyapima mapito yake yote.

  14. Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?

  15. Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?

  16. Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.

  17. Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.

  18. Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke

  19. wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.

  20. Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.

  21. (Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;

  22. mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)

  23. Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:

  24. “Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.

  25. Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!