Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Psalms

896 mistari · 16 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.

  2. Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.

  3. Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.

  4. Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?

  5. Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.

  6. Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”

  7. Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.

  8. Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,

  9. “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”

  10. Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.

  11. Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.

  12. Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”

  13. Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.

  14. Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.

  15. Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.

  16. Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!

  17. Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”

  18. Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.

  19. Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.

  20. Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.

  21. Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.

  22. Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.

  23. Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

  24. Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi. Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.

  25. Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu kuwa aibu mpaka lini? Mtapenda udanganyifu na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?