Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Pride

303 mistari · 61 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa waendao mbali na amri zako.

  2. Ingawa wenye majivuno wamenisingizia uongo, nitafuata mausia yako kwa moyo wangu wote.

  3. Mioyo yao ni katili na migumu, bali mimi napendezwa na sheria yako.

  4. Wenye majivuno na waaibishwe kwa kunikosea mimi bila sababu, lakini mimi nitatafakari juu ya mausia yako.

  5. Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Moyo wangu hauna kiburi, Ee Bwana, macho yangu hayajivuni; sijishughulishi na mambo makuu kunizidi wala mambo ya ajabu mno kwangu.

  6. Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.

  7. Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.

  8. Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:

  9. macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,

  10. “Mimi hekima, nakaa pamoja na busara; ninamiliki maarifa na busara.

  11. Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; ninachukia kiburi na majivuno, tabia mbaya na mazungumzo potovu.

  12. Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.

  13. Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.

  14. Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.

  15. Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.

  16. Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.

  17. Kiburi huzalisha magomvi tu, bali hekima hupatikana kwa wale wanaozingatia ushauri.

  18. Yeye anayemdharau jirani yake hutenda dhambi, bali amebarikiwa yeye aliye na huruma kwa mhitaji.

  19. Mpumbavu hubeza maonyo ya baba yake, bali yeyote akubaliye maonyo huonyesha busara.

  20. Adhabu kali humngoja yeye aachaye njia; yeye achukiaye maonyo atakufa.

  21. Mwenye mzaha huchukia maonyo; hatataka shauri kwa mwenye hekima.

  22. Bwana hubomoa nyumba ya mtu mwenye kiburi, bali huilinda mipaka ya mjane isiguswe.

  23. Yeye anayedharau maonyo hujidharau mwenyewe, bali yeyote anayekubali maonyo hupata ufahamu.

  24. Bwana huwachukia sana wote wenye kiburi cha moyo. Uwe na hakika kwa hili: Hawataepuka kuadhibiwa.

  25. Kiburi hutangulia maangamizi, roho ya majivuno hutangulia maanguko.