Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Afflictions and Adversities

526 mistari · 5 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.

  2. Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.

  3. Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.

  4. Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.

  5. Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.

  6. Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.

  7. Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.

  8. “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

  9. Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.

  10. Anapochukua kwa ghafula, ni nani awezaye kumzuia? Ni nani awezaye kumwambia, ‘Unafanya nini?’

  11. Hata kama ningemwita kwenye shauri, naye akakubali, siamini kama angenisikiliza.

  12. Yeye angeniangamiza kwa dhoruba na kuongeza majeraha yangu pasipo na sababu.

  13. Asingeniacha nipumue bali angenifunika kabisa na huzuni kuu.

  14. Kama ni suala la nguvu, yeye ni mwenye nguvu! Kama ni suala la haki, ni nani awezaye kumwita mahakamani?

  15. Hata kama sikuwa na hatia, kinywa changu kingenihukumu; kama sikuwa na kosa, kingenitangaza kuwa mwenye hatia.

  16. “Ingawa mimi sina kosa, haileti tofauti katika nafsi yangu; nauchukia uhai wangu.

  17. Hayo yote ni sawa; ndiyo sababu nasema, ‘Yeye huwaangamiza wasio na makosa pamoja na waovu.’

  18. Wakati pigo liletapo kifo cha ghafula, yeye hudhihaki kule kukata tamaa kwa yule asiye na kosa.

  19. Wakati nchi inapoangukia mikononi mwa waovu, yeye huwafunga macho mahakimu wake. Kama si yeye, basi ni nani?

  20. “Siku zangu zapita mbio kuliko mkimbiaji; zinapita upesi bila kuona furaha hata kidogo.

  21. Zinapita upesi kama mashua ya mafunjo, mfano wa tai ayashukiaye mawindo kwa ghafula.

  22. Kama nikisema, ‘Nitayasahau malalamiko yangu, nitabadili sura ya uso wangu na kutabasamu,’

  23. bado ninahofia mateso yangu yote, kwa kuwa ninajua hutanihesabu kuwa sina hatia.

  24. Kwa kuwa nimeonekana mwenye hatia, kwa nini basi nitaabishwe bure?

  25. Hata kama ningejiosha kwa sabuni na kutakasa mikono yangu kwa magadi,