Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 17:11takriban 33 BK

    Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.

  2. Yohana 17:12takriban 33 BK

    Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.

  3. Yohana 17:13takriban 33 BK

    “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.

  4. Yohana 17:14takriban 33 BK

    Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.

  5. Yohana 17:15takriban 33 BK

    Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.

  6. Yohana 17:16takriban 33 BK

    Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.

  7. Yohana 17:17takriban 33 BK

    Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.

  8. Yohana 17:18takriban 33 BK

    Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.

  9. Yohana 17:19takriban 33 BK

    Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.

  10. Yohana 17:20takriban 33 BK

    “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao

  11. Yohana 17:21takriban 33 BK

    ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.

  12. Yohana 17:22takriban 33 BK

    Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.

  13. Yohana 17:23takriban 33 BK

    Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.

  14. Yohana 17:24takriban 33 BK

    “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.

  15. Yohana 17:25takriban 33 BK

    “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.

  16. Yohana 17:26takriban 33 BK

    Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”

  17. Yohana 18:1takriban 33 BK

    Yesu alipomaliza kuomba, akaondoka na wanafunzi wake wakavuka Bonde la Kidroni. Upande wa pili palikuwa na bustani, yeye na wanafunzi wake wakaingia humo.

  18. Yohana 18:2takriban 33 BK

    Basi Yuda, yule aliyemsaliti alipafahamu mahali hapo kwani Yesu alikuwa akikutana humo na wanafunzi wake mara kwa mara.

  19. Yohana 18:3takriban 33 BK

    Hivyo Yuda akaja bustanini. Aliongoza kikosi cha askari wa Kirumi, na baadhi ya maafisa kutoka kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo. Nao walikuwa wamechukua taa, mienge na silaha.

  20. Yohana 18:4takriban 33 BK

    Yesu akijua yale yote yatakayompata, akajitokeza mbele yao akawauliza, “Mnamtafuta nani?”

  21. Yohana 18:5takriban 33 BK

    Wao wakamjibu, “Yesu wa Nazareti.” Yesu akawajibu, “Mimi ndiye.” Yuda, yule aliyemsaliti alikuwa amesimama pamoja nao.

  22. Yohana 18:6takriban 33 BK

    Yesu alipowaambia, “Mimi ndiye,” walirudi nyuma na kuanguka chini!

  23. Yohana 18:7takriban 33 BK

    Akawauliza tena, “Mnamtafuta nani?” Nao wakamjibu, “Yesu wa Nazareti.”

  24. Yohana 18:8takriban 33 BK

    Yesu akawaambia, “Nimekwisha kuwaambia kuwa, mimi ndiye; kwa hiyo kama mnanitafuta mimi, waacheni hawa watu waende zao.”

  25. Yohana 18:9takriban 33 BK

    Hii ilikuwa ili litimie lile neno alilosema, “Sikumpoteza hata mmoja miongoni mwa wale ulionipa.”