Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Yohana 15:21takriban 33 BK

    Watawatendea ninyi haya yote kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu hawamjui yeye aliyenituma.

  2. Yohana 15:22takriban 33 BK

    Kama sikuja na kusema nao wasingalikuwa na hatia ya dhambi. Lakini sasa hawana udhuru kwa ajili ya dhambi zao.

  3. Yohana 15:23takriban 33 BK

    Yeyote anayenichukia mimi, anamchukia pia na Baba yangu.

  4. Yohana 15:24takriban 33 BK

    Kama sikuwa nimefanya miujiza ambayo haijapata kufanywa na mtu mwingine yeyote, wasingalikuwa na hatia ya dhambi. Lakini sasa wameiona miujiza hii na bado wakatuchukia mimi na Baba yangu.

  5. Yohana 15:25takriban 33 BK

    Lakini hii ni kutimiza lile neno lililoandikwa kwenye Sheria kwamba, ‘Walinichukia pasipo sababu.’

  6. Yohana 15:26takriban 33 BK

    “Lakini atakapokuja huyo Msaidizi nitakayemtuma kwenu kutoka kwa Baba, yaani, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia mimi.

  7. Yohana 15:27takriban 33 BK

    Ninyi nanyi itawapasa kushuhudia kwa sababu mmekuwa pamoja nami tangu mwanzo.

  8. Yohana 16:1takriban 33 BK

    “Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani.

  9. Yohana 16:2takriban 33 BK

    Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu.

  10. Yohana 16:3takriban 33 BK

    Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.

  11. Yohana 16:4takriban 33 BK

    Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.

  12. Yohana 16:5takriban 33 BK

    “Sasa mimi ninakwenda kwake yeye aliyenituma, lakini hakuna hata aniulizaye, ‘Unakwenda wapi?’

  13. Yohana 16:6takriban 33 BK

    Kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni.

  14. Yohana 16:7takriban 33 BK

    Lakini nawaambia kweli, yafaa mimi niondoke, kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, lakini nikienda nitamtuma kwenu.

  15. Yohana 16:8takriban 33 BK

    Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu.

  16. Yohana 16:9takriban 33 BK

    Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi,

  17. Yohana 16:10takriban 33 BK

    kwa habari ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena,

  18. Yohana 16:11takriban 33 BK

    kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.

  19. Yohana 16:12takriban 33 BK

    “Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa.

  20. Yohana 16:13takriban 33 BK

    Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo.

  21. Yohana 16:14takriban 33 BK

    Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.

  22. Yohana 16:15takriban 33 BK

    Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.

  23. Yohana 16:16takriban 33 BK

    “Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.”

  24. Yohana 16:17takriban 33 BK

    Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? Naye ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninakwenda kwa Baba’?”

  25. Yohana 16:18takriban 33 BK

    Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Kitambo kidogo’? Hatuelewi hilo analosema.”