Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 18:7takriban 33 BK

    Je, Mungu hatawatendea haki wateule wake wanaomlilia usiku na mchana? Je, atakawia kuwasaidia?

  2. Luka 18:8takriban 33 BK

    Ninawaambia, atawapatia haki upesi. Lakini je, Mwana wa Adamu atakapokuja ataikuta imani duniani?”

  3. Luka 18:9takriban 33 BK

    Yesu akatoa mfano huu kwa wale waliojiamini kuwa wao ni wenye haki na kuwadharau wengine:

  4. Luka 18:10takriban 33 BK

    “Watu wawili walikwenda Hekaluni kusali, mmoja wao alikuwa Farisayo na mwingine alikuwa mtoza ushuru.

  5. Luka 18:11takriban 33 BK

    Yule Farisayo, akasimama, akasali hivi na kuomba kwake mwenyewe: ‘Mungu, nakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wengine ambao ni wanyangʼanyi, wadhalimu, na wazinzi, wala kama huyu mtoza ushuru.

  6. Luka 18:12takriban 33 BK

    Mimi nafunga mara mbili kwa juma, na natoa sehemu ya kumi ya mapato yangu.’

  7. Luka 18:13takriban 33 BK

    “Lakini yule mtoza ushuru akasimama mbali, wala hakuthubutu hata kuinua uso wake kutazama mbinguni, bali alijipigapiga kifuani na kusema: ‘Mungu, nihurumie, mimi mwenye dhambi.’

  8. Luka 18:14takriban 33 BK

    “Nawaambia, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amehesabiwa haki mbele za Mungu zaidi ya yule Farisayo. Kwa maana yeyote ajikwezaye atashushwa, na yeyote ajishushaye atakwezwa.”

  9. Luka 18:15takriban 33 BK

    Pia, watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wachanga ili awaguse. Wanafunzi wake walipoona hivyo, wakawakemea.

  10. Luka 18:16takriban 33 BK

    Lakini Yesu akawaita wale watoto waje kwake, akasema, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.

  11. Luka 18:17takriban 33 BK

    Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”

  12. Luka 18:18takriban 33 BK

    Mtawala mmoja akamuuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”

  13. Luka 18:19takriban 33 BK

    Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.

  14. Luka 18:20takriban 33 BK

    Unazijua amri: ‘Usizini, usiue, usiibe, usishuhudie uongo, waheshimu baba yako na mama yako.’ ”

  15. Luka 18:21takriban 33 BK

    Akajibu, “Amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”

  16. Luka 18:22takriban 33 BK

    Yesu aliposikia haya, akamwambia, “Bado kuna jambo moja ulilopungukiwa. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”

  17. Luka 18:23takriban 33 BK

    Aliposikia jambo hili, alisikitika sana kwa maana alikuwa mtu mwenye mali nyingi.

  18. Luka 18:24takriban 33 BK

    Yesu akamtazama, akasema, “Tazama jinsi ilivyo vigumu kwa tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!

  19. Luka 18:25takriban 33 BK

    Hakika ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”

  20. Luka 18:26takriban 33 BK

    Wale waliosikia haya wakauliza, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”

  21. Luka 18:27takriban 33 BK

    Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa wanadamu yanawezekana kwa Mungu.”

  22. Luka 18:28takriban 33 BK

    Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha vyote tulivyokuwa navyo tukakufuata!”

  23. Luka 18:29takriban 33 BK

    Yesu akajibu, “Amin, nawaambia, hakuna hata mtu aliyeacha nyumba yake, au mke, au ndugu, au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu

  24. Luka 18:30takriban 33 BK

    ambaye hatapewa mara nyingi zaidi ya hivyo katika maisha haya, na hatimaye kupata uzima wa milele ujao.”

  25. Luka 18:31takriban 33 BK

    Yesu akawachukua wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na kila kitu kilichoandikwa na manabii kumhusu Mwana wa Adamu kitatimizwa.