circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Luka 16:25takriban 33 BK
“Lakini Abrahamu akamjibu, ‘Mwanangu, kumbuka kwamba wakati wa uhai wako ulipata mambo mazuri, lakini Lazaro alipata mambo mabaya. Lakini sasa anafarijiwa hapa na wewe uko katika maumivu makuu.
- Luka 16:26takriban 33 BK
Zaidi ya hayo, kati yetu na ninyi huko kumewekwa shimo kubwa, ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko wasiweze, wala mtu yeyote asiweze kuvuka kutoka huko kuja kwetu.’
- Luka 16:27takriban 33 BK
“Akasema, ‘Basi, nakuomba, umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu,
- Luka 16:28takriban 33 BK
maana ninao ndugu watano. Awaonye, ili wasije nao wakafika mahali hapa pa mateso.’
- Luka 16:29takriban 33 BK
“Abrahamu akamjibu, ‘Ndugu zako wana Maandiko ya Mose na Manabii, wawasikilize hao.’
- Luka 16:30takriban 33 BK
“Yule tajiri akasema, ‘Hapana, baba Abrahamu, lakini mtu kutoka kwa wafu akiwaendea, watatubu.’
- Luka 16:31takriban 33 BK
“Abrahamu akamwambia, ‘Kama wasipowasikiliza Mose na Manabii, hawataweza kushawishika hata kama mtu akifufuka kutoka kwa wafu.’ ”
- Luka 17:1takriban 33 BK
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mambo yanayosababisha watu watende dhambi hayana budi kutukia. Lakini ole wake mtu yule anayeyasababisha.
- Luka 17:2takriban 33 BK
Ingekuwa heri kama mtu huyo angefungiwa jiwe la kusagia shingoni na kutoswa baharini, kuliko kumsababisha mmojawapo wa hawa wadogo kutenda dhambi.
- Luka 17:3takriban 33 BK
Kwa hiyo, jilindeni. “Kama ndugu yako akikukosea mwonye, naye akitubu, msamehe.
- Luka 17:4takriban 33 BK
Kama akikukosea mara saba kwa siku moja na mara saba kwa siku moja akaja kwako akisema, ‘Ninatubu,’ msamehe.”
- Luka 17:5takriban 33 BK
Mitume wake wakamwambia Bwana, “Tuongezee imani.”
- Luka 17:6takriban 33 BK
Bwana akawajibu, “Kama mkiwa na imani ndogo kama punje ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu, ‘Ngʼoka ukaote baharini,’ nao ungewatii.
- Luka 17:7takriban 33 BK
“Ikiwa mmoja wenu ana mtumishi anayelima shambani au anayechunga kondoo, je, mtumishi huyo arudipo atamwambia, ‘Karibu hapa keti ule chakula?’
- Luka 17:8takriban 33 BK
Je, badala yake, hatamwambia, ‘Niandalie chakula, nile, jifunge unitumikie ninapokula na kunywa; baadaye waweza kula na kunywa?’
- Luka 17:9takriban 33 BK
Je, huyo mtu atamshukuru mtumishi huyo kwa kutimiza yale aliyoamriwa?
- Luka 17:10takriban 33 BK
Vivyo hivyo nanyi mkiisha kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi tu watumishi tusiostahili; tumefanya tu yale tuliyopaswa kufanya.’ ”
- Luka 17:11takriban 33 BK
Yesu alipokuwa njiani akienda Yerusalemu, alipitia mpakani mwa Samaria na Galilaya.
- Luka 17:12takriban 33 BK
Alipokuwa akiingia kwenye kijiji kimoja, watu kumi waliokuwa na ukoma wakakutana naye. Wakasimama mbali,
- Luka 17:13takriban 33 BK
wakapaza sauti, wakasema, “Yesu, Bwana, tuhurumie!”
- Luka 17:14takriban 33 BK
Alipowaona akawaambia, “Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani.” Nao walipokuwa njiani wakienda, wakatakasika.
- Luka 17:15takriban 33 BK
Mmoja wao alipoona kwamba amepona, akarudi kwa Yesu, akimsifu Mungu kwa sauti kuu.
- Luka 17:16takriban 33 BK
Akajitupa miguuni mwa Yesu akamshukuru. Yeye alikuwa Msamaria.
- Luka 17:17takriban 33 BK
Yesu akauliza, “Je, hawakutakaswa wote kumi? Wako wapi wale wengine tisa?
- Luka 17:18takriban 33 BK
Hakuna hata mmoja aliyeonekana kurudi ili kumshukuru Mungu isipokuwa huyu mgeni?”