Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 17:19takriban 33 BK

    Yesu akamwambia, “Inuka na uende zako, imani yako imekuponya.”

  2. Luka 17:20takriban 33 BK

    Yesu alipoulizwa na Mafarisayo Ufalme wa Mungu utakuja lini, yeye akawajibu, “Ufalme wa Mungu hauji kwa kuchunguza kwa bidii,

  3. Luka 17:21takriban 33 BK

    wala watu hawatasema, ‘Huu hapa,’ au ‘Ule kule,’ kwa maana Ufalme wa Mungu umo ndani yenu.”

  4. Luka 17:22takriban 33 BK

    Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Wakati utafika ambapo mtatamani kuiona moja ya siku ya Mwana wa Adamu, lakini hamtaiona.

  5. Luka 17:23takriban 33 BK

    Watu watawaambia, ‘Yule kule!’ Au, ‘Huyu hapa!’ Msiwakimbilie.

  6. Luka 17:24takriban 33 BK

    Kwa maana kama vile umeme wa radi umulikavyo katika anga kuanzia mwisho mmoja hadi mwingine, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.

  7. Luka 17:25takriban 33 BK

    Lakini kwanza itampasa kuteseka katika mambo mengi na kukataliwa na kizazi hiki.

  8. Luka 17:26takriban 33 BK

    “Kama ilivyokuwa siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Adamu.

  9. Luka 17:27takriban 33 BK

    Watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia katika safina. Ndipo gharika ikaja na kuwaangamiza wote.

  10. Luka 17:28takriban 33 BK

    “Ndivyo ilivyokuwa katika siku za Loti: Watu walikuwa wakila na kunywa, wakinunua na kuuza, wakilima na kujenga.

  11. Luka 17:29takriban 33 BK

    Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, ikanyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni ukawaangamiza wote.

  12. Luka 17:30takriban 33 BK

    “Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Adamu atakapofunuliwa.

  13. Luka 17:31takriban 33 BK

    Siku hiyo, mtu yeyote aliye juu ya dari ya nyumba yake, hata vitu vyake vikiwa ndani ya hiyo nyumba, asishuke kuvichukua. Vivyo hivyo mtu aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua chochote.

  14. Luka 17:32takriban 33 BK

    Mkumbukeni mke wa Loti!

  15. Luka 17:33takriban 33 BK

    Mtu yeyote anayejaribu kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayeyapoteza maisha yake atayaokoa.

  16. Luka 17:34takriban 33 BK

    Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa wamelala kitanda kimoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa.

  17. Luka 17:35takriban 33 BK

    Wanawake wawili watakuwa wanasaga nafaka pamoja; naye mmoja atatwaliwa na mwingine ataachwa. [

  18. Luka 17:36takriban 33 BK

    Wanaume wawili watakuwa wanafanya kazi pamoja shambani; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.]”

  19. Luka 17:37takriban 33 BK

    Kisha wakamuuliza, “Haya yatatukia wapi Bwana?” Akawaambia, “Pale ulipo mzoga, huko ndiko tai watakapokusanyika.”

  20. Luka 18:1takriban 33 BK

    Kisha Yesu akawapa wanafunzi wake mfano ili kuwaonyesha kuwa yawapasa kuomba pasipo kukata tamaa.

  21. Luka 18:2takriban 33 BK

    Akawaambia, “Katika mji mmoja alikuwepo hakimu ambaye hakumwogopa Mungu wala kumjali mtu.

  22. Luka 18:3takriban 33 BK

    Katika mji huo alikuwako mjane mmoja ambaye alikuwa akija kwake mara kwa mara akimwomba, ‘Tafadhali nipatie haki kati yangu na adui yangu.’

  23. Luka 18:4takriban 33 BK

    “Kwa muda mrefu yule hakimu alikataa. Lakini hatimaye akasema moyoni mwake, ‘Ijapokuwa simwogopi Mungu wala simjali mwanadamu,

  24. Luka 18:5takriban 33 BK

    lakini kwa kuwa huyu mjane ananisumbuasumbua, nitahakikisha amepata haki yake ili asiendelee kunichosha kwa kunijia mara kwa mara!’ ”

  25. Luka 18:6takriban 33 BK

    Bwana akasema, “Sikilizeni asemavyo huyu hakimu dhalimu.