Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Luka 19:14takriban 33 BK

    “Lakini raiya wa nchi yake walimchukia wakapeleka ujumbe na kusema, ‘Hatutaki huyu mtu awe mfalme wetu.’

  2. Luka 19:15takriban 33 BK

    “Hata hivyo alirudi akiwa amekwisha kupokea mamlaka ya ufalme, akawaita wale watumishi wake aliokuwa amewaachia fedha, ili afahamu ni faida kiasi gani kila mmoja wao aliyopata kwa kufanya biashara.

  3. Luka 19:16takriban 33 BK

    “Wa kwanza akaja na kusema, ‘Bwana, kutokana na fedha uliyoniachia, nimepata faida mara kumi zaidi.’

  4. Luka 19:17takriban 33 BK

    “Yule bwana akamjibu, ‘Umefanya vizuri mtumishi mwema! Kwa sababu umekuwa mwaminifu katika wajibu mdogo sana, nakupa mamlaka juu ya miji kumi.’

  5. Luka 19:18takriban 33 BK

    “Wa pili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, fedha yako imeleta faida mara tano zaidi.’

  6. Luka 19:19takriban 33 BK

    “Bwana wake akajibu, ‘Nakupa mamlaka juu ya miji mitano.’

  7. Luka 19:20takriban 33 BK

    “Kisha akaja yule mtumishi mwingine, akasema, ‘Bwana, hii hapa fedha yako. Niliitunza vizuri kwenye kitambaa.

  8. Luka 19:21takriban 33 BK

    Nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu. Unachukua ambapo hukuweka kitu, na unavuna mahali ambapo hukupanda kitu.’

  9. Luka 19:22takriban 33 BK

    “Bwana wake akamjibu, ‘Nitakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, wewe mtumishi mwovu! Kama ulifahamu kwamba mimi ni mtu mgumu, nichukuaye mahali ambapo sikuweka kitu na kuvuna mahali ambapo sikupanda,

  10. Luka 19:23takriban 33 BK

    kwa nini basi hukuweka fedha zangu kwa watoa riba, ili nitakaporudi nichukue iliyo yangu na riba yake?’

  11. Luka 19:24takriban 33 BK

    “Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama karibu, ‘Mnyangʼanyeni fungu lake la fedha, mkampe yule mwenye kumi.’

  12. Luka 19:25takriban 33 BK

    “Wakamwambia, ‘Bwana, mbona; tayari anayo mafungu kumi!’

  13. Luka 19:26takriban 33 BK

    “Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.

  14. Luka 19:27takriban 33 BK

    Lakini wale adui zangu ambao hawakutaka mimi niwe mfalme juu yao. Waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’ ”

  15. Luka 19:28takriban 33 BK

    Baada ya Yesu kusema haya, alitangulia kupanda kwenda Yerusalemu.

  16. Luka 19:29takriban 33 BK

    Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima uitwao Mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili, akawaambia,

  17. Luka 19:30takriban 33 BK

    “Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.

  18. Luka 19:31takriban 33 BK

    Kama mtu akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’ ”

  19. Luka 19:32takriban 33 BK

    Wale waliotumwa wakaenda, wakakuta kila kitu kama vile Yesu alivyokuwa amewaambia.

  20. Luka 19:33takriban 33 BK

    Walipokuwa wanamfungua yule mwana-punda, wenyewe wakawauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwana-punda?”

  21. Luka 19:34takriban 33 BK

    Wale wanafunzi wakajibu, “Bwana anamhitaji.”

  22. Luka 19:35takriban 33 BK

    Wakamleta kwa Yesu, nao baada ya kutandika mavazi yao juu ya huyo mwana-punda, wakampandisha Yesu juu yake.

  23. Luka 19:36takriban 33 BK

    Alipokuwa akienda akiwa amempanda, watu wakatandaza mavazi yao barabarani.

  24. Luka 19:37takriban 33 BK

    Alipokaribia mahali yanapoanzia materemko ya Mlima wa Mizeituni, umati wote wa wafuasi wake wakaanza kumsifu Mungu kwa furaha kwa sauti kuu kwa ajili ya matendo yote ya miujiza waliyoyaona. Wakasema:

  25. Luka 19:38takriban 33 BK

    “Amebarikiwa Mfalme ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amani mbinguni na utukufu huko juu sana.”