circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Luka 20:16takriban 33 BK
Atakuja na kuwaua hao wapangaji, na kuwapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia hayo wakasema, “Mungu apishie mbali jambo hili lisitokee!”
- Luka 20:17takriban 33 BK
Lakini Yesu akawakazia macho, akasema, “Basi ni nini maana ya yale yaliyoandikwa: “ ‘Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?
- Luka 20:18takriban 33 BK
Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
- Luka 20:19takriban 33 BK
Walimu wa sheria na viongozi wa makuhani wakatafuta njia ya kumkamata mara moja, kwa sababu walifahamu kwamba amesema mfano huo kwa ajili yao. Lakini waliwaogopa watu.
- Luka 20:20takriban 33 BK
Kwa hiyo wakawa wanamchunguza na kutuma wapelelezi waliojifanya kuwa wenye haki ili wapate kumtega kwa maneno asemayo, ili wamtie katika uwezo na mamlaka ya mtawala.
- Luka 20:21takriban 33 BK
Hivyo wale wapelelezi wakamuuliza, “Mwalimu, tunajua unasema na kufundisha yaliyo kweli wala humpendelei mtu, bali wafundisha njia ya Mungu katika kweli.
- Luka 20:22takriban 33 BK
Je, ni halali sisi kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
- Luka 20:23takriban 33 BK
Lakini Yesu akatambua hila yao, kwa hiyo akawaambia,
- Luka 20:24takriban 33 BK
“Nionyesheni dinari. Je, sura hii na maandishi haya yaliyoko juu yake ni vya nani?”
- Luka 20:25takriban 33 BK
Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Akawaambia, “Basi mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
- Luka 20:26takriban 33 BK
Wakashindwa kumkamata kwa yale aliyokuwa amesema hadharani. Nao wakashangazwa mno na majibu yake, wakanyamaza kimya.
- Luka 20:27takriban 33 BK
Baadhi ya Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza,
- Luka 20:28takriban 33 BK
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
- Luka 20:29takriban 33 BK
Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa, akafa bila kuzaa mtoto.
- Luka 20:30takriban 33 BK
Kisha yule wa pili akamwoa huyo mjane, naye akafa bila mtoto,
- Luka 20:31takriban 33 BK
naye wa tatu pia akamwoa. Vivyo hivyo ndugu wote saba wakawa wamemwoa huyo mwanamke, na wote wakafa pasipo yeyote kupata mtoto.
- Luka 20:32takriban 33 BK
Mwishowe, yule mwanamke naye akafa.
- Luka 20:33takriban 33 BK
Sasa basi, siku ya ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
- Luka 20:34takriban 33 BK
Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa.
- Luka 20:35takriban 33 BK
Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi.
- Luka 20:36takriban 33 BK
Hawa hawawezi kufa tena, kwa maana wao ni kama malaika. Wao ni watoto wa Mungu, kwa sababu ni watoto wa ufufuo.
- Luka 20:37takriban 33 BK
Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila kuteketea, alipomwita Bwana, ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.’
- Luka 20:38takriban 33 BK
Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa kuwa kwake wote ni hai.”
- Luka 20:39takriban 33 BK
Baadhi ya walimu wa sheria wakasema, “Mwalimu, umesema sawasawa kabisa!”
- Luka 20:40takriban 33 BK
Baada ya hayo hakuna mtu aliyethubutu kumuuliza maswali tena.