Rukia maudhui

circa 1446 BC

Sinai & The Law

God meets Israel at Mount Sinai, reveals the Ten Commandments, and establishes the Tabernacle and the priestly covenant.

1,657 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Kutoka 19:22takriban 1491 KK

    Hata makuhani, watakaomkaribia Bwana ni lazima wajiweke wakfu, la sivyo Bwana atawaadhibu.”

  2. Kutoka 19:23takriban 1491 KK

    Mose akamwambia Bwana, “Watu hawawezi kupanda mlima Sinai kwa sababu wewe mwenyewe ulituonya ukisema, ‘Wekeni mipaka kuuzunguka mlima na kuutenga kama patakatifu.’ ”

  3. Kutoka 19:24takriban 1491 KK

    Bwana akajibu, “Shuka ukamlete Aroni pamoja nawe. Lakini makuhani pamoja na watu wasije wakalazimisha kuja kwa Bwana, nisije nikawaadhibu.”

  4. Kutoka 19:25takriban 1491 KK

    Basi Mose akashuka kwa watu na kuwaambia lile aliloambiwa.

  5. Kutoka 20:1takriban 1491 KK

    Ndipo Mungu akasema maneno haya yote:

  6. Kutoka 20:2takriban 1491 KK

    “Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa Misri, kutoka nchi ya utumwa.

  7. Kutoka 20:3takriban 1491 KK

    Usiwe na miungu mingine ila mimi.

  8. Kutoka 20:4takriban 1491 KK

    Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni, au duniani chini, au ndani ya maji.

  9. Kutoka 20:5takriban 1491 KK

    Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,

  10. Kutoka 20:6takriban 1491 KK

    lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.

  11. Kutoka 20:7takriban 1491 KK

    Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.

  12. Kutoka 20:8takriban 1491 KK

    Ikumbuke siku ya Sabato, uitakase.

  13. Kutoka 20:9takriban 1491 KK

    Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote,

  14. Kutoka 20:10takriban 1491 KK

    lakini siku ya saba ni Sabato kwa Bwana Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wako wa kiume au wa kike, wala wanyama wako, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.

  15. Kutoka 20:11takriban 1491 KK

    Kwa kuwa kwa siku sita, Bwana aliumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo, lakini akapumzika siku ya saba. Kwa hiyo Bwana akaibariki siku ya Sabato na kuifanya takatifu.

  16. Kutoka 20:12takriban 1491 KK

    Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.

  17. Kutoka 20:13takriban 1491 KK

    Usiue.

  18. Kutoka 20:14takriban 1491 KK

    Usizini.

  19. Kutoka 20:15takriban 1491 KK

    Usiibe.

  20. Kutoka 20:16takriban 1491 KK

    Usimshuhudie jirani yako uongo.

  21. Kutoka 20:17takriban 1491 KK

    Usiitamani nyumba ya jirani yako. Usimtamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wa kiume au wa kike, wala ngʼombe wake au punda wake, wala chochote kile alicho nacho jirani yako.”

  22. Kutoka 20:18takriban 1491 KK

    Watu walipoona ngurumo na radi, na kusikia mlio wa tarumbeta, na kuuona mlima katika moshi, walitetemeka kwa woga. Wakasimama mbali

  23. Kutoka 20:19takriban 1491 KK

    na wakamwambia Mose, “Sema nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza. Lakini usimwache Mungu aseme nasi, la sivyo tutakufa.”

  24. Kutoka 20:20takriban 1491 KK

    Mose akawaambia watu, “Msiogope! Mungu amekuja kuwajaribu, ili kwamba hofu ya Mungu iwakalie, msitende dhambi.”

  25. Kutoka 20:21takriban 1491 KK

    Watu wakabaki mbali, wakati Mose alipolisogelea lile giza nene mahali pale Mungu alipokuwa.