Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 2 Timotheo 3:3takriban 66 BK

    wasio na upendo, wasiopenda kupatanishwa, wasingiziaji, wasiozuia tamaa zao, wakatili, wasiopenda mema,

  2. 2 Timotheo 3:4takriban 66 BK

    wasaliti, wakaidi, waliojaa majivuno, wapendao anasa zaidi kuliko kumpenda Mungu:

  3. 2 Timotheo 3:5takriban 66 BK

    wakiwa na mfano wa utauwa kwa nje, lakini wakizikana nguvu za Mungu. Jiepushe na watu wa namna hiyo.

  4. 2 Timotheo 3:6takriban 66 BK

    Miongoni mwao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu na kuwachukua mateka wanawake wajinga, waliolemewa na dhambi zao na kuyumbishwa na aina zote za tamaa mbaya.

  5. 2 Timotheo 3:7takriban 66 BK

    Wakijifunza siku zote lakini kamwe wasiweze kufikia ujuzi wa kweli.

  6. 2 Timotheo 3:8takriban 66 BK

    Kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Mose, vivyo hivyo watu hawa hupingana na ile kweli. Hawa ni watu wenye akili zilizopotoka, ambao wamekataliwa kwa mambo ya imani.

  7. 2 Timotheo 3:9takriban 66 BK

    Lakini hawataendelea sana, kwa sababu upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama ulivyokuwa dhahiri upumbavu wa hao watu wawili.

  8. 2 Timotheo 3:10takriban 66 BK

    Lakini wewe umeyajua mafundisho yangu, mwenendo, makusudi, imani, uvumilivu, upendo, ustahimilivu,

  9. 2 Timotheo 3:11takriban 66 BK

    mateso na taabu, yaani mambo yote yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Listra, mateso yote niliyostahimili, lakini Bwana aliniokoa katika hayo yote.

  10. 2 Timotheo 3:12takriban 66 BK

    Naam, yeyote anayetaka kuishi maisha ya utauwa ndani ya Kristo Yesu atateswa.

  11. 2 Timotheo 3:13takriban 66 BK

    Lakini watu waovu na wadanganyaji watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.

  12. 2 Timotheo 3:14takriban 66 BK

    Bali wewe, udumu katika yale uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti, ukitambua ya kuwa ulijifunza hayo kutoka kwa nani,

  13. 2 Timotheo 3:15takriban 66 BK

    na jinsi ambavyo tangu utoto umeyajua Maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha upate wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.

  14. 2 Timotheo 3:16takriban 66 BK

    Kila Andiko limevuviwa na Mungu na lafaa kwa mafundisho, kwa kuwaonya watu makosa yao, kwa kuwaongoza na kwa kuwafundisha katika haki,

  15. 2 Timotheo 3:17takriban 66 BK

    ili mtu wa Mungu awe amekamilishwa, apate kutenda kila kazi njema.

  16. 2 Timotheo 4:1takriban 66 BK

    Nakuagiza mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu watu walio hai na waliokufa wakati wa kuja kwake na ufalme wake, kwamba:

  17. 2 Timotheo 4:2takriban 66 BK

    Hubiri Neno; kuwa tayari wakati ufaao na wakati usiofaa; karipia, kemea na utie moyo kwa uvumilivu wote na kwa mafundisho mazuri.

  18. 2 Timotheo 4:3takriban 66 BK

    Maana wakati utakuja watu watakapokataa kuyakubali mafundisho yenye uzima. Badala yake, ili kutimiza tamaa zao wenyewe, watajikusanyia idadi kubwa ya walimu wapate kuwaambia yale ambayo masikio yao yanayowasha yanatamani kuyasikia.

  19. 2 Timotheo 4:4takriban 66 BK

    Watakataa kusikiliza kweli na kuzigeukia hadithi za uongo.

  20. 2 Timotheo 4:5takriban 66 BK

    Kwa habari yako wewe, vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiza wajibu wote wa huduma yako.

  21. 2 Timotheo 4:6takriban 66 BK

    Kwa maana mimi sasa ni tayari kumiminwa kama sadaka ya kinywaji, nayo saa yangu ya kuondoka imetimia.

  22. 2 Timotheo 4:7takriban 66 BK

    Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.

  23. 2 Timotheo 4:8takriban 66 BK

    Sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanitunukia siku ile: wala si mimi tu, bali pia wote ambao wamengoja kwa shauku kudhihirishwa kwake.

  24. 2 Timotheo 4:9takriban 66 BK

    Jitahidi kuja kwangu upesi

  25. 2 Timotheo 4:10takriban 66 BK

    kwa sababu Dema, kwa kuupenda ulimwengu, ameniacha na amekwenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia na Tito amekwenda Dalmatia.