Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Waefeso 5:2takriban 64 BK

    mkiishi maisha ya upendo, kama vile Kristo alivyotupenda sisi akajitoa kwa ajili yetu kuwa sadaka yenye harufu nzuri na dhabihu kwa Mungu.

  2. Waefeso 5:3takriban 64 BK

    Lakini uasherati, usitajwe miongoni mwenu, wala uchafu wa aina yoyote, wala tamaa, kwa sababu mambo haya hayastahili miongoni mwa watakatifu.

  3. Waefeso 5:4takriban 64 BK

    Wala pasiwepo mazungumzo machafu ya aibu, au maneno ya upuzi au mzaha, ambayo hayafai, badala yake mshukuruni Mungu.

  4. Waefeso 5:5takriban 64 BK

    Kwa habari ya mambo haya mjue hakika kwamba: Msherati, wala mtu mwovu, wala mwenye tamaa mbaya, mtu kama huyo ni mwabudu sanamu, kamwe hataurithi Ufalme wa Kristo na wa Mungu.

  5. Waefeso 5:6takriban 64 BK

    Mtu yeyote na asiwadanganye kwa maneno matupu, kwa kuwa hasira ya Mungu huwaka kwa sababu ya mambo kama haya juu ya wale wasiomtii.

  6. Waefeso 5:7takriban 64 BK

    Kwa hiyo, msishirikiane nao.

  7. Waefeso 5:8takriban 64 BK

    Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru

  8. Waefeso 5:9takriban 64 BK

    (kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli),

  9. Waefeso 5:10takriban 64 BK

    nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana.

  10. Waefeso 5:11takriban 64 BK

    Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.

  11. Waefeso 5:12takriban 64 BK

    Kwa maana ni aibu hata kutaja mambo yale ambayo wasiotii wanayafanya sirini.

  12. Waefeso 5:13takriban 64 BK

    Lakini kila kitu kilichowekwa nuruni, huonekana,

  13. Waefeso 5:14takriban 64 BK

    kwa kuwa nuru ndiyo hufanya kila kitu kionekane. Hii ndiyo sababu imesemekana: “Amka, wewe uliyelala, ufufuke kutoka kwa wafu, naye Kristo atakuangazia.”

  14. Waefeso 5:15takriban 64 BK

    Kwa hiyo angalieni sana jinsi mnavyoenenda, si kama watu wasio na hekima, bali kama wenye hekima,

  15. Waefeso 5:16takriban 64 BK

    mkiukomboa wakati, kwa sababu nyakati hizi ni za uovu.

  16. Waefeso 5:17takriban 64 BK

    Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini mapenzi ya Bwana.

  17. Waefeso 5:18takriban 64 BK

    Pia msilewe kwa mvinyo, ambamo ndani yake mna upotovu, bali mjazwe Roho.

  18. Waefeso 5:19takriban 64 BK

    Msemezane ninyi kwa ninyi kwa zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia na kumsifu Bwana mioyoni mwenu,

  19. Waefeso 5:20takriban 64 BK

    siku zote mkimshukuru Mungu Baba kwa kila jambo katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo.

  20. Waefeso 5:21takriban 64 BK

    Nyenyekeaneni ninyi kwa ninyi kwa heshima kwa ajili ya Kristo.

  21. Waefeso 5:22takriban 64 BK

    Ninyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana.

  22. Waefeso 5:23takriban 64 BK

    Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe kama vile Kristo alivyo kichwa cha Kanisa, ambalo ni mwili wake, naye Kristo ni Mwokozi wake.

  23. Waefeso 5:24takriban 64 BK

    Basi, kama vile Kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo na wake nao imewapasa kuwatii waume zao kwa kila jambo.

  24. Waefeso 5:25takriban 64 BK

    Ninyi waume, wapendeni wake zenu, kama vile Kristo alivyolipenda Kanisa akajitoa kwa ajili yake

  25. Waefeso 5:26takriban 64 BK

    kusudi alifanye takatifu, akilitakasa kwa kuliosha kwa maji katika Neno lake,