circa AD 48–96
Letters to the Churches
Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.
Mistari ya kipindi hiki
- Waefeso 5:2takriban 64 BK
mkiishi maisha ya upendo, kama vile Kristo alivyotupenda sisi akajitoa kwa ajili yetu kuwa sadaka yenye harufu nzuri na dhabihu kwa Mungu.
- Waefeso 5:3takriban 64 BK
Lakini uasherati, usitajwe miongoni mwenu, wala uchafu wa aina yoyote, wala tamaa, kwa sababu mambo haya hayastahili miongoni mwa watakatifu.
- Waefeso 5:4takriban 64 BK
Wala pasiwepo mazungumzo machafu ya aibu, au maneno ya upuzi au mzaha, ambayo hayafai, badala yake mshukuruni Mungu.
- Waefeso 5:5takriban 64 BK
Kwa habari ya mambo haya mjue hakika kwamba: Msherati, wala mtu mwovu, wala mwenye tamaa mbaya, mtu kama huyo ni mwabudu sanamu, kamwe hataurithi Ufalme wa Kristo na wa Mungu.
- Waefeso 5:6takriban 64 BK
Mtu yeyote na asiwadanganye kwa maneno matupu, kwa kuwa hasira ya Mungu huwaka kwa sababu ya mambo kama haya juu ya wale wasiomtii.
- Waefeso 5:7takriban 64 BK
Kwa hiyo, msishirikiane nao.
- Waefeso 5:8takriban 64 BK
Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru
- Waefeso 5:9takriban 64 BK
(kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli),
- Waefeso 5:10takriban 64 BK
nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana.
- Waefeso 5:11takriban 64 BK
Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.
- Waefeso 5:12takriban 64 BK
Kwa maana ni aibu hata kutaja mambo yale ambayo wasiotii wanayafanya sirini.
- Waefeso 5:13takriban 64 BK
Lakini kila kitu kilichowekwa nuruni, huonekana,
- Waefeso 5:14takriban 64 BK
kwa kuwa nuru ndiyo hufanya kila kitu kionekane. Hii ndiyo sababu imesemekana: “Amka, wewe uliyelala, ufufuke kutoka kwa wafu, naye Kristo atakuangazia.”
- Waefeso 5:15takriban 64 BK
Kwa hiyo angalieni sana jinsi mnavyoenenda, si kama watu wasio na hekima, bali kama wenye hekima,
- Waefeso 5:16takriban 64 BK
mkiukomboa wakati, kwa sababu nyakati hizi ni za uovu.
- Waefeso 5:17takriban 64 BK
Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini mapenzi ya Bwana.
- Waefeso 5:18takriban 64 BK
Pia msilewe kwa mvinyo, ambamo ndani yake mna upotovu, bali mjazwe Roho.
- Waefeso 5:19takriban 64 BK
Msemezane ninyi kwa ninyi kwa zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia na kumsifu Bwana mioyoni mwenu,
- Waefeso 5:20takriban 64 BK
siku zote mkimshukuru Mungu Baba kwa kila jambo katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
- Waefeso 5:21takriban 64 BK
Nyenyekeaneni ninyi kwa ninyi kwa heshima kwa ajili ya Kristo.
- Waefeso 5:22takriban 64 BK
Ninyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana.
- Waefeso 5:23takriban 64 BK
Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe kama vile Kristo alivyo kichwa cha Kanisa, ambalo ni mwili wake, naye Kristo ni Mwokozi wake.
- Waefeso 5:24takriban 64 BK
Basi, kama vile Kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo na wake nao imewapasa kuwatii waume zao kwa kila jambo.
- Waefeso 5:25takriban 64 BK
Ninyi waume, wapendeni wake zenu, kama vile Kristo alivyolipenda Kanisa akajitoa kwa ajili yake
- Waefeso 5:26takriban 64 BK
kusudi alifanye takatifu, akilitakasa kwa kuliosha kwa maji katika Neno lake,