circa AD 48–96
Letters to the Churches
Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.
Mistari ya kipindi hiki
- Waefeso 5:27takriban 64 BK
apate kujiletea Kanisa tukufu lisilo na doa wala kunyanzi au waa lolote, bali takatifu na lisilo na hatia.
- Waefeso 5:28takriban 64 BK
Vivyo hivyo imewapasa waume kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
- Waefeso 5:29takriban 64 BK
Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake mwenyewe, bali huulisha na kuutunza vizuri, kama Kristo anavyolitunza Kanisa lake.
- Waefeso 5:30takriban 64 BK
Sisi tu viungo vya mwili wake.
- Waefeso 5:31takriban 64 BK
“Kwa sababu hii, mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
- Waefeso 5:32takriban 64 BK
Siri hii ni kubwa, bali mimi nanena kuhusu Kristo na Kanisa.
- Waefeso 5:33takriban 64 BK
Hata hivyo, kila mmoja wenu ampende mkewe kama anavyoipenda nafsi yake mwenyewe, naye mke lazima amheshimu mumewe.
- Waefeso 6:1takriban 64 BK
Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa kuwa hili ni jema.
- Waefeso 6:2takriban 64 BK
“Waheshimu baba yako na mama yako,” hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi,
- Waefeso 6:3takriban 64 BK
“upate baraka na uishi siku nyingi duniani.”
- Waefeso 6:4takriban 64 BK
Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, bali waleeni kwa nidhamu na mafundisho ya Bwana.
- Waefeso 6:5takriban 64 BK
Ninyi watumwa, watiini hao walio mabwana zenu hapa duniani kwa heshima na kwa kutetemeka na kwa moyo mmoja, kama vile mnavyomtii Kristo.
- Waefeso 6:6takriban 64 BK
Watiini, si tu wakati wakiwaona ili mpate upendeleo wao, bali mtumike kama watumwa wa Kristo, mkifanya mapenzi ya Mungu kwa moyo.
- Waefeso 6:7takriban 64 BK
Tumikeni kwa moyo wote, kama vile mnamtumikia Bwana na si wanadamu.
- Waefeso 6:8takriban 64 BK
Mkijua kwamba Bwana atampa kila mtu thawabu kwa lolote jema alilotenda, kama yeye ni mtumwa au ni mtu huru.
- Waefeso 6:9takriban 64 BK
Nanyi mabwana, watendeeni watumwa wenu kwa jinsi iyo hiyo. Msiwatishe, kwa kuwa mnajua ya kwamba yeye aliye Bwana wenu na Bwana wao yuko mbinguni, naye hana upendeleo.
- Waefeso 6:10takriban 64 BK
Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.
- Waefeso 6:11takriban 64 BK
Vaeni silaha zote za Mungu ili kwamba mweze kuzipinga hila za ibilisi.
- Waefeso 6:12takriban 64 BK
Kwa maana kushindana kwetu si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
- Waefeso 6:13takriban 64 BK
Kwa hiyo vaeni silaha zote za Mungu ili mweze kushindana siku ya uovu itakapokuja nanyi mkiisha kufanya yote, simameni imara.
- Waefeso 6:14takriban 64 BK
Kwa hiyo simameni imara mkiwa mmejifunga kweli kiunoni na kuvaa dirii ya haki kifuani,
- Waefeso 6:15takriban 64 BK
nayo miguu yenu ifungiwe utayari tuupatao kwa Injili ya amani.
- Waefeso 6:16takriban 64 BK
Zaidi ya haya yote, twaeni ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
- Waefeso 6:17takriban 64 BK
Vaeni chapeo ya wokovu na mchukue upanga wa Roho, ambao ni Neno la Mungu.
- Waefeso 6:18takriban 64 BK
Mkiomba kwa Roho siku zote katika sala zote na maombi, mkikesha kila wakati mkiwaombea watakatifu wote.