Rukia maudhui

circa 1406–1380 BC

Conquest of Canaan

Joshua leads Israel across the Jordan into the promised land, defeating the Canaanite kingdoms one by one.

658 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Yoshua 12:22takriban 1450 KK

    mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja

  2. Yoshua 12:23takriban 1450 KK

    mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja

  3. Yoshua 12:24takriban 1450 KK

    mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.

  4. Yoshua 13:1takriban 1444 KK

    Yoshua alipokuwa mzee na umri wake ukiwa umesogea sana, Bwana akamwambia, “Wewe ni mzee sana, na bado kumesalia sehemu kubwa sana za nchi ambazo ni za kutwaliwa.

  5. Yoshua 13:2takriban 1444 KK

    “Nchi iliyosalia ni hii: maeneo yote ya Wafilisti na Wageshuri:

  6. Yoshua 13:3takriban 1444 KK

    kutoka Mto Shihori ulioko mashariki mwa Misri, kuelekea kaskazini kwenye eneo la Ekroni, ambayo yote ilihesabika kama ya Wakanaani (maeneo yale matano ya watawala wa Kifilisti, ambayo ni Gaza, Ashdodi, Ashkeloni, Gathi na Ekroni: ndiyo nchi ya Waavi);

  7. Yoshua 13:4takriban 1444 KK

    kuanzia kusini, nchi yote ya Wakanaani, kuanzia Ara ambayo ni ya Wasidoni, ikienea hadi Afeki, na eneo la Waamori,

  8. Yoshua 13:5takriban 1444 KK

    eneo la Wagebali; Lebanoni yote kuelekea mashariki, kuanzia Baal-Gadi chini ya Mlima Hermoni hadi Lebo-Hamathi.

  9. Yoshua 13:6takriban 1444 KK

    “Na kuhusu wakaaji wote katika maeneo ya milima, kuanzia Lebanoni hadi Misrefoth-Maimu, pamoja na eneo lote la Wasidoni, mimi mwenyewe nitawafukuza watoke mbele ya Waisraeli. Hakikisha umegawa nchi hii kwa Israeli kuwa urithi, kama nilivyokuagiza,

  10. Yoshua 13:7takriban 1444 KK

    sasa basi, ligawanye eneo hili kwa yale makabila tisa na ile nusu ya kabila la Manase kuwa urithi.”

  11. Yoshua 13:8takriban 1444 KK

    Ile nusu nyingine ya Manase, Wareubeni na Wagadi, walishapokea urithi Mose aliokuwa amewapa mashariki mwa Yordani, sawasawa na mtumishi wa Bwana alivyowagawia.

  12. Yoshua 13:9takriban 1444 KK

    Eneo lao lilienea toka Aroeri, iliyoko ukingoni mwa Bonde la Arnoni kuanzia mji ulio katikati ya bonde, likijumlisha nchi ya uwanda wa juu wote wa Medeba mpaka Diboni,

  13. Yoshua 13:10takriban 1444 KK

    nayo miji yote ya Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi mpakani mwa Waamoni.

  14. Yoshua 13:11takriban 1444 KK

    Vilevile ilijumlisha Gileadi, eneo la Wageshuri na Wamaaka, mlima wote wa Hermoni na Bashani yote ikienea hadi Saleka:

  15. Yoshua 13:12takriban 1444 KK

    yaani ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyekuwa ametawala katika Ashtarothi na Edrei, na ndiye pekee alisalia kwa Warefai. Mose alikuwa amewashinda na kuteka nchi yao.

  16. Yoshua 13:13takriban 1444 KK

    Lakini Waisraeli hawakuwafukuza watu wa Geshuri na wa Maaka, kwa hiyo wanaendelea kuishi miongoni mwa Waisraeli mpaka leo hii.

  17. Yoshua 13:14takriban 1444 KK

    Lakini kwa kabila la Lawi, Mose hakupeana urithi, kwa kuwa sadaka za kuteketezwa kwa moto zilizotolewa kwa Bwana, Mungu wa Israeli, ndizo zilizokuwa urithi wao, kama alivyowaahidi.

  18. Yoshua 13:15takriban 1444 KK

    Haya ndiyo maeneo ambayo Mose alikuwa amewapa kabila la Reubeni ukoo kwa ukoo:

  19. Yoshua 13:16takriban 1444 KK

    Eneo la Aroeri lililo ukingoni mwa Bonde la Arnoni, na kuanzia mji ulio katikati ya bonde, pia uwanda wote wa juu kupita Medeba

  20. Yoshua 13:17takriban 1444 KK

    hadi Heshboni na miji yake yote kwenye uwanda wa juu, ikijumlishwa miji ya Diboni, Bamoth-Baali, Beth-Baal-Meoni,

  21. Yoshua 13:18takriban 1444 KK

    Yahasa, Kedemothi, Mefaathi,

  22. Yoshua 13:19takriban 1444 KK

    Kiriathaimu, Sibma, Sereth-Shahari juu ya kilima kilicho katika bonde,

  23. Yoshua 13:20takriban 1444 KK

    Beth-Peori, materemko ya Pisga na Beth-Yeshimothi:

  24. Yoshua 13:21takriban 1444 KK

    miji yote ya uwanda wa juu na eneo lote la utawala wa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala katika Heshboni. Mose alikuwa amemshinda Sihoni, pia watawala wakuu wa Wamidiani, ambao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba, waliokuwa wameungana na Sihoni, ambao waliishi katika nchi ile.

  25. Yoshua 13:22takriban 1444 KK

    Pamoja na wale waliouawa katika vita, Waisraeli walikuwa wamemuua kwa upanga Balaamu mwana wa Beori aliyekuwa mchawi.