Rukia maudhui

circa 1406–1380 BC

Conquest of Canaan

Joshua leads Israel across the Jordan into the promised land, defeating the Canaanite kingdoms one by one.

658 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Yoshua 11:20takriban 1450 KK

    Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

  2. Yoshua 11:21takriban 1450 KK

    Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.

  3. Yoshua 11:22takriban 1450 KK

    Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.

  4. Yoshua 11:23takriban 1450 KK

    Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.

  5. Yoshua 12:1takriban 1450 KK

    Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:

  6. Yoshua 12:2takriban 1450 KK

    Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.

  7. Yoshua 12:3takriban 1450 KK

    Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.

  8. Yoshua 12:4takriban 1450 KK

    Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.

  9. Yoshua 12:5takriban 1450 KK

    Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.

  10. Yoshua 12:6takriban 1450 KK

    Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.

  11. Yoshua 12:7takriban 1450 KK

    Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:

  12. Yoshua 12:8takriban 1450 KK

    nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):

  13. Yoshua 12:9takriban 1450 KK

    mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja

  14. Yoshua 12:10takriban 1450 KK

    mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja

  15. Yoshua 12:11takriban 1450 KK

    mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja

  16. Yoshua 12:12takriban 1450 KK

    mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja

  17. Yoshua 12:13takriban 1450 KK

    mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja

  18. Yoshua 12:14takriban 1450 KK

    mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja

  19. Yoshua 12:15takriban 1450 KK

    mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja

  20. Yoshua 12:16takriban 1450 KK

    mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja

  21. Yoshua 12:17takriban 1450 KK

    mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja

  22. Yoshua 12:18takriban 1450 KK

    mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja

  23. Yoshua 12:19takriban 1450 KK

    mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja

  24. Yoshua 12:20takriban 1450 KK

    mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja

  25. Yoshua 12:21takriban 1450 KK

    mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja