- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
circa 1406–1380 BC
Conquest of Canaan
Joshua leads Israel across the Jordan into the promised land, defeating the Canaanite kingdoms one by one.
Mistari ya kipindi hiki
- Yoshua 11:20takriban 1450 KK
Kwa maana Bwana mwenyewe ndiye aliifanya mioyo yao iwe migumu, ili kupigana vita dhidi ya Israeli ili apate kuwafutilia mbali pasipo huruma, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
- Yoshua 11:21takriban 1450 KK
Wakati huo Yoshua akaenda kuwaangamiza Waanaki kutoka nchi ya vilima: kuanzia Hebroni, Debiri na Anabu, na kutoka nchi yote ya vilima ya Yuda na kutoka nchi yote ya vilima ya Israeli. Yoshua akawaangamiza kabisa pamoja na miji yao.
- Yoshua 11:22takriban 1450 KK
Hawakubaki Waanaki wowote katika nchi ya Israeli, ila tu katika nchi ya Gaza, Gathi na Ashdodi.
- Yoshua 11:23takriban 1450 KK
Hivyo Yoshua akaiteka nchi hiyo yote kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose, naye Yoshua akawapa Israeli kuwa urithi wao, kulingana na walivyogawanyika katika kabila zao. Ndipo nchi ikawa na amani bila vita.
- Yoshua 12:1takriban 1450 KK
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
- Yoshua 12:2takriban 1450 KK
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
- Yoshua 12:3takriban 1450 KK
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
- Yoshua 12:4takriban 1450 KK
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
- Yoshua 12:5takriban 1450 KK
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
- Yoshua 12:6takriban 1450 KK
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
- Yoshua 12:7takriban 1450 KK
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
- Yoshua 12:8takriban 1450 KK
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
- Yoshua 12:9takriban 1450 KK
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
- Yoshua 12:10takriban 1450 KK
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
- Yoshua 12:11takriban 1450 KK
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
- Yoshua 12:12takriban 1450 KK
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
- Yoshua 12:13takriban 1450 KK
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
- Yoshua 12:14takriban 1450 KK
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
- Yoshua 12:15takriban 1450 KK
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
- Yoshua 12:16takriban 1450 KK
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
- Yoshua 12:17takriban 1450 KK
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
- Yoshua 12:18takriban 1450 KK
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
- Yoshua 12:19takriban 1450 KK
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
- Yoshua 12:20takriban 1450 KK
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
- Yoshua 12:21takriban 1450 KK
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja