Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Sickness

120 mistari · 47 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.

  2. Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.

  3. Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.

  4. “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,

  5. kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:

  6. Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.

  7. Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe, kwa haki yako uniokoe.

  8. Nitegee sikio lako, uje uniokoe haraka; uwe kwangu mwamba wa kimbilio, ngome imara ya kuniokoa.

  9. Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu, uniongoze na kunilinda kwa ajili ya jina lako.

  10. Uniepushe na mtego niliotegewa, maana wewe ndiwe kimbilio langu.

  11. Ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako, unikomboe Ee Bwana, uliye Mungu wa kweli.

  12. Ninawachukia wale wanaongʼangʼania sanamu batili; mimi ninamtumaini Bwana.

  13. Nitafurahia na kushangilia upendo wako, kwa kuwa uliona mateso yangu na ulijua maumivu ya nafsi yangu.

  14. Hukunikabidhi kwa adui yangu bali umeiweka miguu yangu mahali penye nafasi.

  15. Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia na nikajinyenyekesha kwa kufunga. Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,

  16. Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.

  17. Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.

  18. Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.

  19. Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,

  20. wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.

  21. Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.

  22. Zaburi ya Daudi. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Vyote vilivyomo ndani yangu vilihimidi jina lake takatifu.

  23. Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, wala usisahau wema wake wote,

  24. akusamehe dhambi zako zote, akuponya magonjwa yako yote,

  25. Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.