Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Sickness: Acknowledge that, comes from God

10 mistari · 47 vipengele

Mistari kuhusu Acknowledge that, comes from God

  1. Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe, kwa haki yako uniokoe.

  2. Nitegee sikio lako, uje uniokoe haraka; uwe kwangu mwamba wa kimbilio, ngome imara ya kuniokoa.

  3. Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu, uniongoze na kunilinda kwa ajili ya jina lako.

  4. Uniepushe na mtego niliotegewa, maana wewe ndiwe kimbilio langu.

  5. Ninaikabidhi roho yangu mikononi mwako, unikomboe Ee Bwana, uliye Mungu wa kweli.

  6. Ninawachukia wale wanaongʼangʼania sanamu batili; mimi ninamtumaini Bwana.

  7. Nitafurahia na kushangilia upendo wako, kwa kuwa uliona mateso yangu na ulijua maumivu ya nafsi yangu.

  8. Hukunikabidhi kwa adui yangu bali umeiweka miguu yangu mahali penye nafasi.

  9. Kama hema la mchunga mifugo, nyumba yangu imebomolewa na kutwaliwa kutoka kwangu. Kama mfumaji nimevingirisha maisha yangu, naye amenikatilia mbali kutoka kitanda cha mfumi. Mchana na usiku uliyakomesha maisha yangu.

  10. Lakini niseme nini? Amesema nami, naye yeye mwenyewe amelitenda hili. Nitatembea kwa unyenyekevu katika miaka yangu yote kwa sababu ya haya maumivu makali ya nafsi yangu.