Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Sickness: Often manifests saving grace to sinners during

11 mistari · 47 vipengele

Mistari kuhusu Often manifests saving grace to sinners during

  1. Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,

  2. kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.

  3. Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.

  4. Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.

  5. “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,

  6. kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:

  7. Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.

  8. Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.

  9. Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.

  10. Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.

  11. Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.