Rukia maudhui

circa 1446–1406 BC

The Wilderness Years

Forty years of wandering in the desert test Israel's faith and prepare a new generation to enter the promised land.

2,247 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Hesabu 11:31takriban 1490 KK

    Kisha ukatokea upepo kutoka kwa Bwana, nao ukawaletea kware kutoka baharini. Ukawaangusha kwenye eneo lote linalozunguka kambi na kujaa ardhini kimo cha mita moja hivi kutoka ardhini kwenye eneo la umbali wa mwendo wa siku moja kila upande.

  2. Hesabu 11:32takriban 1490 KK

    Mchana kutwa na usiku kucha pamoja na siku nzima iliyofuata watu walitoka kwenda kuokota kware. Hakuna mtu yeyote aliyekusanya chini ya homeri kumi. Kisha wakazianika kuzunguka kambi yote.

  3. Hesabu 11:33takriban 1490 KK

    Lakini walipokuwa wakila nyama, ilipokuwa ingali kati ya meno yao na kabla hawajamaliza kula, hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya watu, naye akawapiga kwa tauni.

  4. Hesabu 11:34takriban 1490 KK

    Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Kibroth-Hataava, kwa sababu huko ndiko walipowazika watu ambao walitamani sana chakula kingine.

  5. Hesabu 11:35takriban 1490 KK

    Kutoka Kibroth-Hataava watu wakasafiri mpaka Haserothi na kukaa huko.

  6. Hesabu 12:1takriban 1490 KK

    Miriamu na Aroni walianza kuzungumza dhidi ya Mose kwa sababu ya mke wake Mkushi, kwa kuwa alikuwa ameoa Mkushi.

  7. Hesabu 12:2takriban 1490 KK

    Waliuliza, “Je, Bwana amesema kupitia Mose peke yake? Je, hajasema kutupitia sisi pia?” Naye Bwana akasikia hili.

  8. Hesabu 12:3takriban 1490 KK

    (Basi Mose alikuwa mtu mnyenyekevu sana, mnyenyekevu kuliko mtu mwingine yeyote katika uso wa dunia.)

  9. Hesabu 12:4takriban 1490 KK

    Ghafula Bwana akawaambia Mose, Aroni na Miriamu, “Njooni katika Hema la Kukutania, ninyi nyote watatu.” Kwa hiyo wote watatu wakaenda.

  10. Hesabu 12:5takriban 1490 KK

    Kisha Bwana akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye ingilio la Hema, akawaita Aroni na Miriamu. Wakati wote wawili waliposogea mbele,

  11. Hesabu 12:6takriban 1490 KK

    Bwana akasema, “Sikilizeni maneno yangu: “Akiwapo nabii wa Bwana miongoni mwenu, nitajifunua kwake kwa maono, nitanena naye katika ndoto.

  12. Hesabu 12:7takriban 1490 KK

    Lakini sivyo kwa mtumishi wangu Mose; yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote.

  13. Hesabu 12:8takriban 1490 KK

    Kwake nitanena naye uso kwa uso, waziwazi wala si kwa mafumbo; yeye ataona umbo la Bwana. Kwa nini basi ninyi hamkuogopa kuzungumza kinyume cha mtumishi wangu Mose?”

  14. Hesabu 12:9takriban 1490 KK

    Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao, akawaacha.

  15. Hesabu 12:10takriban 1490 KK

    Wakati hilo wingu liliinuka kutoka juu ya Hema, Miriamu akawa tayari ana ukoma, mweupe kama theluji. Aroni akamgeukia, akaona ana ukoma.

  16. Hesabu 12:11takriban 1490 KK

    Kisha Aroni akamwambia Mose, “Tafadhali, bwana wangu, usituhesabie dhambi hii ambayo tumeifanya kwa upumbavu.

  17. Hesabu 12:12takriban 1490 KK

    Usimwache awe kama mtoto mchanga aliyezaliwa akiwa mfu, ambaye nusu ya mwili wake imeharibika hapo atokapo katika tumbo la mama yake.”

  18. Hesabu 12:13takriban 1490 KK

    Hivyo Mose akamlilia Bwana akisema, “Ee Mungu, nakuomba umponye!”

  19. Hesabu 12:14takriban 1490 KK

    Bwana akamjibu Mose, “Je, kama baba yake angemtemea usoni, asingeona aibu kwa siku saba? Mfungie nje ya kambi kwa siku saba; baada ya hapo anaweza kurudishwa kambini.”

  20. Hesabu 12:15takriban 1490 KK

    Kwa hiyo Miriamu akafungiwa nje ya kambi kwa siku saba, nao watu hawakuendelea na safari mpaka aliporudishwa kambini.

  21. Hesabu 12:16takriban 1490 KK

    Baada ya hayo, watu waliondoka Haserothi, wakapiga kambi katika Jangwa la Parani.

  22. Hesabu 13:1takriban 1490 KK

    Bwana akamwambia Mose,

  23. Hesabu 13:2takriban 1490 KK

    “Watume baadhi ya watu wakaipeleleze nchi ya Kanaani, ambayo ninawapa Waisraeli. Kutoka kwa kila kabila la baba zao, tuma mmoja wa viongozi wao.”

  24. Hesabu 13:3takriban 1490 KK

    Hivyo kwa agizo la Bwana Mose akawatuma kutoka Jangwa la Parani. Wote walikuwa viongozi wa Waisraeli.

  25. Hesabu 13:4takriban 1490 KK

    Haya ndiyo majina yao: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;