Rukia maudhui

circa AD 30–62

The Early Church

Pentecost ignites a movement; Peter, Paul, and countless others carry the gospel from Jerusalem to the ends of the earth.

1,007 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Matendo 15:32takriban 51 BK

    Yuda na Sila, ambao wenyewe walikuwa manabii, wakanena maneno mengi ya kuwatia moyo na kuwajenga katika imani wale ndugu walioamini.

  2. Matendo 15:33takriban 51 BK

    Baada ya kukaa huko Antiokia kwa muda, wakaagwa kwa amani na wale ndugu ili waende kwa wale waliowatuma. [

  3. Matendo 15:34takriban 51 BK

    Lakini Sila bado akaendelea kukaa huko.]

  4. Matendo 15:35takriban 51 BK

    Lakini Paulo na Barnaba walibaki Antiokia ambako wao pamoja na wengine wengi walifundisha na kuhubiri neno la Bwana.

  5. Matendo 15:36takriban 51 BK

    Baada ya muda, Paulo akamwambia Barnaba, “Turudi tukawatembelee ndugu katika miji yote tuliyohubiri neno la Bwana tuone jinsi wanavyoendelea.”

  6. Matendo 15:37takriban 51 BK

    Barnaba alitaka wamchukue Yohana aitwaye Marko waende naye.

  7. Matendo 15:38takriban 51 BK

    Lakini Paulo aliona si vyema kwa sababu aliwahi kuwaacha walipokuwa huko Pamfilia, hakutaka kuendelea kufanya kazi naye.

  8. Matendo 15:39takriban 51 BK

    Pakatokea ubishi mkali kati ya Paulo na Barnaba kuhusu jambo hili, hivyo wakagawanyika. Barnaba akamchukua Yohana Marko wakasafiri baharini kwenda Kipro.

  9. Matendo 15:40takriban 51 BK

    Lakini Paulo akamchagua Sila na akaondoka baada ya ndugu kuwatakia neema ya Bwana.

  10. Matendo 15:41takriban 51 BK

    Akapitia Shamu na Kilikia, akiimarisha makanisa ya huko.

  11. Matendo 16:1takriban 53 BK

    Paulo akafika Derbe na kisha Listra, ambako kulikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, ambaye mama yake alikuwa Myahudi aliyeamini, lakini baba yake alikuwa Myunani.

  12. Matendo 16:2takriban 53 BK

    Alikuwa amesifiwa sana na wale ndugu waliokuwa wameamini huko Listra na Ikonio

  13. Matendo 16:3takriban 53 BK

    Paulo alitaka Timotheo afuatane naye, hivyo akamchukua na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi waliokuwa wanaishi eneo lile kwa maana wote walimjua baba yake ni Myunani.

  14. Matendo 16:4takriban 53 BK

    Walipokuwa wakienda mji kwa mji, wakawa wanawapa maamuzi yaliyotolewa na mitume na wazee huko Yerusalemu ili wayafuate.

  15. Matendo 16:5takriban 53 BK

    Hivyo makanisa yakawa imara katika imani na kuongezeka kiidadi kila siku.

  16. Matendo 16:6takriban 53 BK

    Paulo pamoja na wenzake wakasafiri sehemu za Frigia na Galatia, kwa kuwa Roho Mtakatifu hakuwaruhusu kulihubiri neno huko Asia.

  17. Matendo 16:7takriban 53 BK

    Walipofika mpaka wa Misia, wakajaribu kuingia Bithinia lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.

  18. Matendo 16:8takriban 53 BK

    Kwa hiyo wakapita Misia, wakafika Troa.

  19. Matendo 16:9takriban 53 BK

    Wakati wa usiku Paulo akaona maono, mtu wa Makedonia amesimama akimsihi, “Vuka uje huku Makedonia utusaidie.”

  20. Matendo 16:10takriban 53 BK

    Baada ya Paulo kuona maono haya, tulijiandaa kwa haraka kuondoka kwenda Makedonia tukiwa tumesadiki kuwa Mungu alikuwa ametuita kuhubiri habari njema huko.

  21. Matendo 16:11takriban 53 BK

    Tukasafiri kwa njia ya bahari kutoka Troa na kwenda moja kwa moja hadi Samothrake, kesho yake tukafika Neapoli.

  22. Matendo 16:12takriban 53 BK

    Kutoka huko tukasafiri hadi Filipi, mji mkuu wa jimbo hilo la Makedonia, uliokuwa koloni ya Warumi. Nasi tukakaa huko siku kadhaa.

  23. Matendo 16:13takriban 53 BK

    Siku ya Sabato tukaenda nje ya lango la mji kando ya mto, mahali ambapo tulitarajia tungepata mahali pa kufanyia maombi. Tukaketi, tukaanza kuongea na baadhi ya wanawake waliokuwa wamekusanyika huko.

  24. Matendo 16:14takriban 53 BK

    Mmoja wa wale wanawake waliotusikiliza aliitwa Lidia, mfanyabiashara wa nguo za zambarau, mwenyeji wa mji wa Thiatira, aliyekuwa mcha Mungu. Bwana akaufungua moyo wake akaupokea ujumbe wa Paulo.

  25. Matendo 16:15takriban 53 BK

    Basi alipokwisha kubatizwa yeye na watu wa nyumba yake, alitukaribisha nyumbani kwake akisema, “Kama mmeona kweli mimi nimemwamini Bwana, karibuni mkae nyumbani mwangu.” Naye akatushawishi.