Rukia maudhui

circa AD 30–62

The Early Church

Pentecost ignites a movement; Peter, Paul, and countless others carry the gospel from Jerusalem to the ends of the earth.

1,007 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Matendo 7:58takriban 33 BK

    Wakamtupa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka mavazi yao miguuni mwa kijana mmoja ambaye jina lake aliitwa Sauli.

  2. Matendo 7:59takriban 33 BK

    Walipokuwa wakimpiga mawe, Stefano aliomba, “Bwana Yesu, pokea roho yangu.”

  3. Matendo 7:60takriban 33 BK

    Kisha akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa akasema, “Bwana usiwahesabie dhambi hii.” Baada ya kusema hayo, akalala.

  4. Matendo 8:1takriban 34 BK

    Naye Sauli alikuwepo pale, akiridhia kuuawa kwa Stefano. Siku ile kukatukia mateso makuu dhidi ya kanisa huko Yerusalemu, waumini wote isipokuwa mitume wakatawanyika, wakakimbilia Uyahudi na Samaria.

  5. Matendo 8:2takriban 34 BK

    Watu wacha Mungu wakamzika Stefano na kumwombolezea sana.

  6. Matendo 8:3takriban 34 BK

    Lakini kwa habari ya Sauli alikuwa analiharibu kanisa, akiingia nyumba kwa nyumba, akiwaburuta wanawake na wanaume na kuwatupa gerezani.

  7. Matendo 8:4takriban 34 BK

    Kwa hiyo wale waliotawanyika wakalihubiri neno la Mungu kila mahali walipokwenda.

  8. Matendo 8:5takriban 34 BK

    Filipo akateremkia mji mmoja wa Samaria akawahubiria habari za Kristo

  9. Matendo 8:6takriban 34 BK

    Watu walipomsikia Filipo na kuona ishara na miujiza aliyofanya, wakasikiliza kwa bidii yale aliyosema.

  10. Matendo 8:7takriban 34 BK

    Pepo wachafu wakawa wakiwatoka watu wengi huku wakipiga kelele na wengi waliopooza na viwete wakaponywa.

  11. Matendo 8:8takriban 34 BK

    Hivyo pakawa na furaha kuu katika mji huo.

  12. Matendo 8:9takriban 34 BK

    Basi mtu mmoja jina lake Simoni alikuwa amefanya uchawi kwa muda mrefu katika mji huo akiwashangaza watu wote wa Samaria. Alijitapa kwamba yeye ni mtu mkuu,

  13. Matendo 8:10takriban 34 BK

    nao watu wote wakubwa kwa wadogo wakamsikiliza na kumaka, wakisema “Mtu huyu ndiye uweza wa Mungu ujulikanao kama ‘Uweza Mkuu.’ ”

  14. Matendo 8:11takriban 34 BK

    Wakamfuata kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake.

  15. Matendo 8:12takriban 34 BK

    Lakini watu walipomwamini Filipo alipohubiri habari njema za Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, wakabatizwa wanaume na wanawake.

  16. Matendo 8:13takriban 34 BK

    Simoni naye akaamini na akabatizwa. Akamfuata Filipo kila mahali, akistaajabishwa na ishara kuu na miujiza aliyoiona.

  17. Matendo 8:14takriban 34 BK

    Basi mitume waliokuwa Yerusalemu waliposikia kuwa Samaria wamelipokea neno la Mungu, wakawatuma Petro na Yohana waende huko.

  18. Matendo 8:15takriban 34 BK

    Nao walipofika wakawaombea ili wampokee Roho Mtakatifu,

  19. Matendo 8:16takriban 34 BK

    kwa sababu Roho Mtakatifu alikuwa bado hajawashukia hata mmoja ila wamebatizwa tu katika jina la Bwana Yesu.

  20. Matendo 8:17takriban 34 BK

    Ndipo Petro na Yohana wakaweka mikono yao juu ya wale waliobatizwa, nao wakapokea Roho Mtakatifu.

  21. Matendo 8:18takriban 34 BK

    Simoni alipoona kuwa watu wanapokea Roho Mtakatifu mitume walipoweka mikono juu yao, akataka kuwapa fedha

  22. Matendo 8:19takriban 34 BK

    akisema, “Nipeni na mimi uwezo huu ili kila mtu nitakayeweka mikono yangu juu yake apate kupokea Roho Mtakatifu.”

  23. Matendo 8:20takriban 34 BK

    Petro akamjibu, “Fedha yako na iangamie pamoja nawe, kwa sababu ulidhani unaweza kununua karama ya Mungu kwa fedha!

  24. Matendo 8:21takriban 34 BK

    Wewe huna sehemu wala fungu katika huduma hii kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za Mungu.

  25. Matendo 8:22takriban 34 BK

    Kwa hiyo tubu kwa uovu huu wako na umwombe Bwana. Yamkini aweza kukusamehe mawazo uliyo nayo moyoni mwako.