- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Wicked
Mistari muhimu ya Biblia
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.
Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.
Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
Mjinga hafahamu, mpumbavu haelewi,
ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao mabaya wanastawi, wataangamizwa milele.
Hata lini, waovu, Ee Bwana, hata lini waovu watashangilia?
Wanamimina maneno ya kiburi, watenda mabaya wote wamejaa majivuno.
Ee Bwana, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako.
Wanamchinja mjane na mgeni, na kuwaua yatima.
Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”
Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu; enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima?
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.