Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Wicked

724 mistari · 18 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,

  2. nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.

  3. Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.

  4. Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.

  5. Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.

  6. Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.

  7. Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.

  8. Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

  9. Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

  10. Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.

  11. Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.

  12. Mjinga hafahamu, mpumbavu haelewi,

  13. ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao mabaya wanastawi, wataangamizwa milele.

  14. Hata lini, waovu, Ee Bwana, hata lini waovu watashangilia?

  15. Wanamimina maneno ya kiburi, watenda mabaya wote wamejaa majivuno.

  16. Ee Bwana, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako.

  17. Wanamchinja mjane na mgeni, na kuwaua yatima.

  18. Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”

  19. Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu; enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima?

  20. Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,

  21. nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.

  22. Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;

  23. aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.

  24. Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,

  25. Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.