Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu God

662 mistari · 46 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

  2. Lakini kama huyo mtumishi ni mwovu, naye akasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu atakawia muda mrefu,’

  3. kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, na kula na kunywa pamoja na walevi.

  4. Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua.

  5. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wanafiki, mahali ambako kutakuwa ni kulia na kusaga meno.

  6. Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu

  7. Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.”

  8. “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.

  9. Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,

  10. kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani,

  11. ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,

  12. kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:

  13. Kisha Yesu akawaambia mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini uliopandwa katika shamba lake la mizabibu, akaja ili kutafuta tini kwenye mti huo, lakini hakupata hata moja.

  14. Hivyo akamwambia mtunza shamba: ‘Tazama, kwa muda wa miaka mitatu sasa nimekuwa nikija kutafuta matunda kwenye mtini huu, nami sikupata hata moja. Ukate! Kwa nini uendelee kuharibu ardhi?’

  15. “Yule mtunza shamba akamjibu, ‘Bwana, uache tena kwa mwaka mmoja zaidi, nami nitaupalilia na kuuwekea mbolea.

  16. Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vyema, la sivyo uukate.’ ”

  17. “Ikiwa mmoja wenu ana kondoo mia moja, naye akapoteza mmoja wao, je, hawaachi wale tisini na tisa nyikani na kwenda kumtafuta huyo aliyepotea mpaka ampate?

  18. Naye akishampata, humbeba mabegani mwake kwa furaha

  19. na kwenda nyumbani. Kisha huwaita rafiki zake na majirani, na kuwaambia, ‘Furahini pamoja nami; nimempata kondoo wangu aliyepotea.’

  20. Nawaambieni, vivyo hivyo kutakuwa na furaha zaidi mbinguni kwa sababu ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa wenye haki tisini na tisa ambao hawana haja ya kutubu.”

  21. Yesu akaendelea kusema: “Kulikuwa na mtu mmoja aliyekuwa na wana wawili.

  22. Yule mdogo akamwambia baba yake, ‘Baba, nipe urithi wangu.’ Hivyo akawagawia wanawe mali yake.

  23. “Baada ya muda mfupi, yule mdogo akakusanya vitu vyote alivyokuwa navyo, akaenda nchi ya mbali, na huko akaitapanya mali yake kwa maisha ya anasa.

  24. Baada ya kutumia kila kitu alichokuwa nacho, kukawa na njaa kali katika nchi ile yote, naye akawa hana chochote.

  25. Kwa hiyo akaenda akaajiriwa na mwenyeji mmoja wa nchi ile ambaye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.