Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Mathayo 27:41takriban 33 BK

    Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wakamdhihaki wakisema,

  2. Mathayo 27:42takriban 33 BK

    “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe! Yeye ni Mfalme wa Israeli! Ashuke sasa kutoka msalabani, nasi tutamwamini.

  3. Mathayo 27:43takriban 33 BK

    Anamwamini Mungu, basi Mungu na amwokoe sasa kama anamtaka, kwa maana alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu.’ ”

  4. Mathayo 27:44takriban 33 BK

    Hata wale wanyangʼanyi waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana vivyo hivyo.

  5. Mathayo 27:45takriban 33 BK

    Tangu saa sita hadi saa tisa giza liliifunika nchi yote.

  6. Mathayo 27:46takriban 33 BK

    Ilipofika saa tisa, Yesu akapaza sauti akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)

  7. Mathayo 27:47takriban 33 BK

    Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama pale waliposikia hayo, wakasema, “Anamwita Eliya.”

  8. Mathayo 27:48takriban 33 BK

    Ghafula mmoja wao akaenda mbio na kuleta sifongo, akaichovya kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe.

  9. Mathayo 27:49takriban 33 BK

    Wengine wakasema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”

  10. Mathayo 27:50takriban 33 BK

    Yesu alipolia tena kwa sauti kuu, akaitoa roho yake.

  11. Mathayo 27:51takriban 33 BK

    Wakati huo huo pazia la Hekalu likachanika vipande viwili, kuanzia juu hadi chini. Dunia ikatetemeka na miamba ikapasuka.

  12. Mathayo 27:52takriban 33 BK

    Makaburi yakafunguka na miili ya watakatifu waliokuwa wamekufa ikafufuliwa.

  13. Mathayo 27:53takriban 33 BK

    Wakatoka makaburini, na baada ya Yesu kufufuka, waliingia kwenye Mji Mtakatifu na kuwatokea watu wengi.

  14. Mathayo 27:54takriban 33 BK

    Basi yule jemadari na wale waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu walipoona lile tetemeko na yale yote yaliyokuwa yametukia, waliogopa, wakasema, “Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”

  15. Mathayo 27:55takriban 33 BK

    Walikuwako wanawake huko wakiangalia kwa mbali. Hawa walikuwa wamemfuata Yesu tangu Galilaya ili kushughulikia mahitaji yake.

  16. Mathayo 27:56takriban 33 BK

    Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo na Yosefu, na mama yao wana wa Zebedayo.

  17. Mathayo 27:57takriban 33 BK

    Ilipofika jioni, alifika mtu mmoja tajiri kutoka Arimathaya aitwaye Yosefu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.

  18. Mathayo 27:58takriban 33 BK

    Akamwendea Pilato ili kumwomba mwili wa Yesu. Pilato akaamuru apewe.

  19. Mathayo 27:59takriban 33 BK

    Yosefu akauchukua mwili wa Yesu, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi,

  20. Mathayo 27:60takriban 33 BK

    na kuuweka katika kaburi lake mwenyewe jipya, alilokuwa amelichonga kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa katika ingilio la kaburi, akaenda zake.

  21. Mathayo 27:61takriban 33 BK

    Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwepo mahali pale, wakiwa wameketi mkabala na kaburi.

  22. Mathayo 27:62takriban 33 BK

    Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalizi ya Sabato, viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakamwendea Pilato

  23. Mathayo 27:63takriban 33 BK

    na kusema, “Bwana, tumekumbuka kwamba yule mdanganyifu wakati alikuwa bado hai alisema, ‘Baada ya siku tatu nitafufuka.’

  24. Mathayo 27:64takriban 33 BK

    Kwa hiyo uamuru kaburi lilindwe kwa uthabiti mpaka baada ya siku tatu. La sivyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kuuiba mwili wake na kuwaambia watu kwamba amefufuliwa kutoka kwa wafu. Udanganyifu huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”

  25. Mathayo 27:65takriban 33 BK

    Pilato akawaambia, “Ninyi mnao askari walinzi. Nendeni, liwekeeni ulinzi kadri mwezavyo.”