Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Mathayo 26:66takriban 33 BK

    Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”

  2. Mathayo 26:67takriban 33 BK

    Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi

  3. Mathayo 26:68takriban 33 BK

    na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni nani aliyekupiga?”

  4. Mathayo 26:69takriban 33 BK

    Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”

  5. Mathayo 26:70takriban 33 BK

    Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”

  6. Mathayo 26:71takriban 33 BK

    Alipotoka nje kufika kwenye lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwepo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”

  7. Mathayo 26:72takriban 33 BK

    Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”

  8. Mathayo 26:73takriban 33 BK

    Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”

  9. Mathayo 26:74takriban 33 BK

    Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.

  10. Mathayo 26:75takriban 33 BK

    Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.

  11. Mathayo 27:1takriban 33 BK

    Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri pamoja dhidi ya Yesu ili kumuua.

  12. Mathayo 27:2takriban 33 BK

    Wakamfunga, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato, ambaye alikuwa mtawala wa Kirumi.

  13. Mathayo 27:3takriban 33 BK

    Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti Yesu, alipoona kuwa Yesu amehukumiwa, akajuta na akarudisha vile vipande thelathini vya fedha alivyopewa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.

  14. Mathayo 27:4takriban 33 BK

    Akasema, “Nimetenda dhambi, kwa maana nimeisaliti damu isiyo na hatia.” Wakamjibu, “Hilo latuhusu nini sisi? Ni shauri yako.”

  15. Mathayo 27:5takriban 33 BK

    Basi Yuda akavitupa vile vipande vya fedha ndani ya Hekalu akaondoka akaenda kujinyonga.

  16. Mathayo 27:6takriban 33 BK

    Wale viongozi wa makuhani wakazichukua zile fedha wakasema, “Si halali kuchanganya fedha hizi na sadaka kwa sababu hizi ni fedha zenye damu.”

  17. Mathayo 27:7takriban 33 BK

    Kwa hiyo baada ya kushauriana, waliamua kuzitumia kununulia shamba la mfinyanzi, liwe mahali pa kuzikia wageni.

  18. Mathayo 27:8takriban 33 BK

    Hii ndiyo sababu lile shamba likaitwa Shamba la Damu hadi leo.

  19. Mathayo 27:9takriban 33 BK

    Ndipo likatimia lile lililonenwa na nabii Yeremia, kwamba, “Walichukua vile vipande thelathini vya fedha, thamani aliyopangiwa na watu wa Israeli,

  20. Mathayo 27:10takriban 33 BK

    wakanunulia shamba la mfinyanzi, kama vile Bwana alivyoniagiza.”

  21. Mathayo 27:11takriban 33 BK

    Wakati huo Yesu akiwa amesimama mbele ya mtawala, mtawala akamuuliza, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akasema, “Wewe wasema hivyo.”

  22. Mathayo 27:12takriban 33 BK

    Lakini viongozi wa makuhani na wazee walipomshtaki, hakujibu neno.

  23. Mathayo 27:13takriban 33 BK

    Ndipo Pilato akamuuliza, “Je, husikii ni mambo mangapi wanayokushtaki nayo?”

  24. Mathayo 27:14takriban 33 BK

    Lakini Yesu hakumjibu hata kwa shtaka moja, kiasi kwamba mtawala alishangaa sana.

  25. Mathayo 27:15takriban 33 BK

    Basi ilikuwa ni desturi ya mtawala kumfungua mfungwa mmoja aliyechaguliwa na umati wa watu wakati wa sikukuu.