circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Mathayo 26:66takriban 33 BK
Uamuzi wenu ni gani?” Wakajibu, “Anastahili kufa.”
- Mathayo 26:67takriban 33 BK
Kisha wakamtemea mate usoni na wengine wakampiga ngumi. Wengine wakampiga makofi
- Mathayo 26:68takriban 33 BK
na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni nani aliyekupiga?”
- Mathayo 26:69takriban 33 BK
Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
- Mathayo 26:70takriban 33 BK
Lakini Petro akakana mbele yao wote akisema, “Sijui hilo usemalo.”
- Mathayo 26:71takriban 33 BK
Alipotoka nje kufika kwenye lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona, akawaambia watu waliokuwepo, “Huyu mtu alikuwa pamoja na Yesu, Mnazareti.”
- Mathayo 26:72takriban 33 BK
Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi simjui huyo!”
- Mathayo 26:73takriban 33 BK
Baada ya muda mfupi, wale waliokuwa wamesimama pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana usemi wako ni kama wao.”
- Mathayo 26:74takriban 33 BK
Ndipo Petro akaanza kujilaani na kuwaapia, “Mimi simjui mtu huyo!” Papo hapo jogoo akawika.
- Mathayo 26:75takriban 33 BK
Ndipo Petro akakumbuka lile neno Yesu alilokuwa amesema: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
- Mathayo 27:1takriban 33 BK
Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri pamoja dhidi ya Yesu ili kumuua.
- Mathayo 27:2takriban 33 BK
Wakamfunga, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato, ambaye alikuwa mtawala wa Kirumi.
- Mathayo 27:3takriban 33 BK
Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti Yesu, alipoona kuwa Yesu amehukumiwa, akajuta na akarudisha vile vipande thelathini vya fedha alivyopewa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
- Mathayo 27:4takriban 33 BK
Akasema, “Nimetenda dhambi, kwa maana nimeisaliti damu isiyo na hatia.” Wakamjibu, “Hilo latuhusu nini sisi? Ni shauri yako.”
- Mathayo 27:5takriban 33 BK
Basi Yuda akavitupa vile vipande vya fedha ndani ya Hekalu akaondoka akaenda kujinyonga.
- Mathayo 27:6takriban 33 BK
Wale viongozi wa makuhani wakazichukua zile fedha wakasema, “Si halali kuchanganya fedha hizi na sadaka kwa sababu hizi ni fedha zenye damu.”
- Mathayo 27:7takriban 33 BK
Kwa hiyo baada ya kushauriana, waliamua kuzitumia kununulia shamba la mfinyanzi, liwe mahali pa kuzikia wageni.
- Mathayo 27:8takriban 33 BK
Hii ndiyo sababu lile shamba likaitwa Shamba la Damu hadi leo.
- Mathayo 27:9takriban 33 BK
Ndipo likatimia lile lililonenwa na nabii Yeremia, kwamba, “Walichukua vile vipande thelathini vya fedha, thamani aliyopangiwa na watu wa Israeli,
- Mathayo 27:10takriban 33 BK
wakanunulia shamba la mfinyanzi, kama vile Bwana alivyoniagiza.”
- Mathayo 27:11takriban 33 BK
Wakati huo Yesu akiwa amesimama mbele ya mtawala, mtawala akamuuliza, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akasema, “Wewe wasema hivyo.”
- Mathayo 27:12takriban 33 BK
Lakini viongozi wa makuhani na wazee walipomshtaki, hakujibu neno.
- Mathayo 27:13takriban 33 BK
Ndipo Pilato akamuuliza, “Je, husikii ni mambo mangapi wanayokushtaki nayo?”
- Mathayo 27:14takriban 33 BK
Lakini Yesu hakumjibu hata kwa shtaka moja, kiasi kwamba mtawala alishangaa sana.
- Mathayo 27:15takriban 33 BK
Basi ilikuwa ni desturi ya mtawala kumfungua mfungwa mmoja aliyechaguliwa na umati wa watu wakati wa sikukuu.