Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Young Men

347 mistari · 1 kipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Lakini njia ya waovu ni kama giza nene; hawajui kinachowafanya wajikwae.

  2. Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia; sikiliza kwa makini maneno yangu.

  3. Usiruhusu yaondoke machoni pako, yahifadhi ndani ya moyo wako;

  4. kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.

  5. Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo, maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

  6. Epusha kinywa chako na ukaidi; weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.

  7. Macho yako na yatazame mbele, kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.

  8. Sawazisha mapito ya miguu yako na njia zako zote ziwe zimethibitika.

  9. Usigeuke kulia wala kushoto; epusha mguu wako na ubaya.

  10. Mwanangu, sikiliza kwa makini hekima yangu, sikiliza vizuri maneno yangu ya busara,

  11. ili uweze kutunza busara na midomo yako ihifadhi maarifa.

  12. Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba hudondoza asali, na maneno ya kinywa chake ni laini kuliko mafuta;

  13. lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo, mkali kama upanga ukatao kuwili.

  14. Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo; hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.

  15. Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima; njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.

  16. Sasa basi wanangu, nisikilizeni; msiache ninalowaambia.

  17. Njia zenu ziwe mbali naye, msiende karibu na mlango wa nyumba yake,

  18. usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine na miaka yako kwa aliye mkatili,

  19. wageni wasije wakasherehekea utajiri wako na jitihada yako ikatajirisha nyumba ya mwanaume mwingine.

  20. Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu, wakati nyama na mwili wako vimechakaa.

  21. Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu! Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!

  22. Sikuwatii walimu wangu wala kuwasikiliza wakufunzi wangu.

  23. Nimefika ukingoni mwa maangamizi kabisa katikati ya kusanyiko lote.”

  24. Kunywa maji kutoka kwenye kisima chako mwenyewe, maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe.

  25. Je, chemchemi zako zifurike katika barabara za mji na vijito vyako vya maji viwanjani?