Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Young Men

347 mistari · 1 kipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.

  2. Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

  3. Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.

  4. Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.

  5. Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,

  6. yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.

  7. Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,

  8. kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.

  9. Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?

  10. Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?

  11. Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.

  12. Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.

  13. Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.

  14. Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.

  15. Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;

  16. kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.

  17. Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.

  18. Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.

  19. Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.

  20. Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.

  21. Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;

  22. watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.

  23. Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.

  24. Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.

  25. Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke