- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Young Men
Mistari muhimu ya Biblia
Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.
Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu; sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.
Ninawapa mafundisho ya maana, kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.
Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu, ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,
baba alinifundisha akisema, “Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote; yashike maagizo yangu na wewe utaishi.
Pata hekima, pata ufahamu; usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.
Usimwache hekima naye atakuweka salama; mpende, naye atakulinda.
Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima. Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.
Mstahi, naye atakukweza; mkumbatie, naye atakuheshimu.
Atakuvika shada la neema kichwani mwako na kukupa taji ya utukufu.”
Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia, nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
Ninakuongoza katika njia ya hekima na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.
Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa; ukimbiapo, hutajikwaa.
Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; mshike, maana yeye ni uzima wako.
Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu wala usitembee katika njia ya watu wabaya.
Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo; achana nayo, na uelekee njia yako.
Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu; wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.
Wanakula mkate wa uovu, na kunywa mvinyo wa jeuri.
Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko, ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.