- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Young Men
Mistari muhimu ya Biblia
Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
kutega sikio lako kwenye hekima na kuweka moyo wako katika ufahamu,
na kama ukiita busara na kuita kwa sauti ufahamu,
na kama utaitafuta kama fedha na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
ndipo utakapoelewa kumcha Bwana na kupata maarifa ya Mungu.
Kwa maana Bwana hutoa hekima, na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu, yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri.
Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda.
Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,
wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza,
wale wapendao kutenda mabaya na kufurahia upotovu wa ubaya,
ambao mapito yao yamepotoka na ambao ni wapotovu katika njia zao.
Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba, kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno ya kushawishi kutenda ubaya,
aliyemwacha mwenzi wa ujana wake na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.
Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo na mapito yake kwenye roho za waliokufa.
Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi, au kufikia mapito ya uzima.
Hivyo utatembea katika njia za watu wema na kushikamana na mapito ya wenye haki.
Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.
Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi, nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.
Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.